TRENDING
High-flying Hull maintain unbeaten start by holding off Aston Villa in stalemate • Sifuna condemns abduction of Standard Group Associate Editor • Troops discover three decomposing bodies of terrorists in Borno • Qinwen, Potapova spring pair of US Open upsets • Ex-IGP Adamu Wins Nasarawa SDP Gov Ticket, Pledges To Tackle “Misgovernance’ • Athletic Club Thrash Atletico Madrid 3-0 In Stunning  La Liga Rout • Wike To Amaechi: You Have Lost Your Credibility In Politics • 2027: Grassroots Performance, Not Structure, Will Decide Bayelsa West – Olomu • Diphtheria: 68% Of Confirmed Cases Involve Unvaccinated People – NCDC • CAF Confederation Cup: Shooting Stars Secure Narrow First-Leg Win Over CS Sfaxien • Three die, 20 injured in Osun road crash • Makinde says 2027 ambition not limited to region • Lobbying firm replies Keyamo, alleges Tinubu govt pressure over Trump appointment • Ruparelia Group Leads Corporate Backing for India Day 2026 • UPDF Crowned Overall Champions Of 18th Inter-Forces Games In Gulu • FR LAZAR ARASU: Why National Progress is Failing the Rural Woman • Iwobi makes Premier League appearance history • Tinubu’s economic reforms are yielding results — Tope Fasua • Taraba youths capture two suspects over alleged planned attack • Simeone’s Atletico Madrid Crushed 3-0 At Athletic Bilbao • High-flying Hull maintain unbeaten start by holding off Aston Villa in stalemate • Sifuna condemns abduction of Standard Group Associate Editor • Troops discover three decomposing bodies of terrorists in Borno • Qinwen, Potapova spring pair of US Open upsets • Ex-IGP Adamu Wins Nasarawa SDP Gov Ticket, Pledges To Tackle “Misgovernance’ • Athletic Club Thrash Atletico Madrid 3-0 In Stunning  La Liga Rout • Wike To Amaechi: You Have Lost Your Credibility In Politics • 2027: Grassroots Performance, Not Structure, Will Decide Bayelsa West – Olomu • Diphtheria: 68% Of Confirmed Cases Involve Unvaccinated People – NCDC • CAF Confederation Cup: Shooting Stars Secure Narrow First-Leg Win Over CS Sfaxien • Three die, 20 injured in Osun road crash • Makinde says 2027 ambition not limited to region • Lobbying firm replies Keyamo, alleges Tinubu govt pressure over Trump appointment • Ruparelia Group Leads Corporate Backing for India Day 2026 • UPDF Crowned Overall Champions Of 18th Inter-Forces Games In Gulu • FR LAZAR ARASU: Why National Progress is Failing the Rural Woman • Iwobi makes Premier League appearance history • Tinubu’s economic reforms are yielding results — Tope Fasua • Taraba youths capture two suspects over alleged planned attack • Simeone’s Atletico Madrid Crushed 3-0 At Athletic Bilbao
Balozi wa Papa asifia amani ya kidini Tanzania
Back to Home

Balozi wa Papa asifia amani ya kidini Tanzania

Mwananchi about 3 hours 3 mins read
Dar es Salaam. Balozi wa Kitume nchini Tanzania, Askofu Mkuu Angelo Accattino amehitimisha rasmi utume wake Tanzania huku akitaja amani, mshikamano na uelewano wa kidini kuwa miongoni mwa mambo makubwa atakayoyakumbuka baada ya kuondoka nchini. Balozi huyo, ambaye amehudumu nchini tangu Februari 2023, amesema hayo leo Septemba 5, 2026 wakati akitoa salamu katika maadhimisho ya kuwekwa wakfu Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Vicent Mpwaji. Maadhimisho hayo yaliyohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali akiwemo Makamu wa Rais, Deogratius Ndejembi, vyama vya upinzaji akiwemo aliyekuwa Mbunge wa Kisesa mkoani Simiyu, Luhaga Mpina, viongozi wa dini mbalimbali, maaskofu, mapadri, watawa na waamini yaliyofanyika katika viwanja vya Msimbazi Center. Mpwaji alizaliwa Juni 5, 1978 katika Hospitali ya Morogoro, akiwa mtoto wa pili kati ya watoto sita; wavulana wanne na wasichana wawili. Alibatizwa Juni 24, 1978, Morogoro, kabla ya kupokea Komunio ya Kwanza Novemba 26, 1989, Yombo, na Kipaimara Agosti 18, 1991. Akitoa hotuba zake, Accattino amesema maadhimisho hayo yalikuwa ya mwisho kwake kushiriki akiwa Balozi wa Kitume na mwakilishi wa Papa nchini Tanzania kabla ya kuhamishiwa Jamhuri ya Colombia, Amerika Kusini. Amesema anaondoka akibeba picha ya namna Tanzania kama nchi iliyotoa uhuru wa kuabudu kwani alishuhudia namna dini mbalimbali zinavyoishi kwa amani na kuheshimiana. Amesema uwepo wa waamini wanaojaza makanisa na nyumba za ibada za dini mbalimbali pamoja na amani na uelewano uliopo kati ya misingi na mila mbalimbali za kidini umemfanya kutafakari nafasi ya dini katika kujenga jamii. “Imani thabiti, siyo tu ya Wakatoliki bali ya umati wa waamini wanaojaza makanisa na nyumba za ibada za kila namna, pamoja na amani na uelewano uliopo kati ya misingi na mila mbalimbali za kidini, vimenifanya nitafakari,” amesema. Amesema dini inapokuwa na nafasi nzuri katika jamii, inaweza kuwa chombo cha kujenga watu na jamii badala ya kuwa chanzo cha chuki na migogoro.“Jivunieni hili na mlilinde kama zawadi ya amani kubwa zaidi ambayo Mungu amewapa Watanzania,” amesema. Amesema kwa sasa Dar es Salaam imekuwa nyumbani kwake tangu alipowasili nchini Februari 2023, licha ya changamoto ya foleni za magari jijini Dar es Salaam, alilipenda jiji hilo kutokana na ukarimu na uchangamfu wa wakazi wake akitaja pia salamu za kawaida wanazotoa watu barabarani kuwa miongoni mwa mambo atakayoyakumbuka. “Nitahifadhi kumbukumbu za uzuri wa mwonekano wa bahari na fukwe lakini zaidi nitakumbuka watu wake wenye urafiki na uchangamfu,” amesema. Katika hotuba hiyo, Balozi huyo pia alitoa pongezi kwa Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Vicent Mpwaji akimtaka kutumia huduma yake mpya kwa unyenyekevu, uaminifu na upendo. Amesema uteuzi huo unakuja wakati Jimbo Kuu la Dar es Salaam likishuhudia ukuaji wa kasi wa idadi ya waamini na kuanzishwa kwa parokia mpya, hali iliyozalisha hitaji la kupata askofu msaidizi mwingine. Alimtaka Askofu Mpwaji kufuata mfano wa Bikira Maria katika kuitikia wito wa Mungu na kutekeleza majukumu yake ya kichungaji kwa unyenyekevu. “Naomba Mungu aendelee kukujalia neema na baraka tele ili uweze kuwatakasa waamini kwa uaminifu, kuhubiri neno la Mungu na kutoa sakramenti kama mchungaji mwema anayewajali kondoo wake kwa upendo,” amesema. Alitumia nafasi hiyo kuwashukuru viongozi wa Serikali kwa ushirikiano alioupata wakati wa kipindi chake cha uwakilishi wa Baba Mtakatifu nchini, akisema mahusiano kati ya Tanzania na Vatican yaliendelea kuwa mazuri. Amesema alishirikiana na viongozi mbalimbali wa Serikali, hususani mawaziri watatu wa Mambo ya Nje, katika kudumisha mahusiano ya pande mbili kati ya Tanzania na Holy See.

This article was sourced from an external publication.

Share this article
OneClick Africa Logo

Africa's premier digital hub for impactful news, entertainment, and business insights.

© 2026 OneClick Africa. All rights reserved.