TRENDING
Priscilla Ojo & Juma Jux Just Served the Sweetest Matching Traditional Wedding Looks • Delta unveils $100m fund to lure investors as FG backs diversification • NEC approves $4.5bn refinancing of $3.3bn oil-backed loan • 2027: Come, tell Nigerians primary, secondary school you attended – Kalu challenges Tinubu • LAFC co-managing owner Larry Berg voted as next MLS commissioner • Former deputy bureau chief of The Guardian, Anietie Akpan, dies • Nollywood Actress Maureen Okpoko opens up on battle with blindness [VIDEO] • Barca Need A Capable Striker –Flick • Igbo community group in Abuja cautions Southeast leaders against blanket endorsement of Tinubu • I used to borrow to maintain my lifestyle – Timini Egbuson • Arsenal weigh €150m summer move for Vinicius Junior • Okonjo-Iweala says Nigeria needs infrastructure maintenance, not just bigger budgets • Nigeria must deliver competitive barrels to win investment – Seplat’s CEO • NNPP drags INEC, seeks Abdulsalami committee’s intervention over candidates’ nomination • Africa and the imperatives of leadership, By Toyin Falola • APC kicks off campaign ahead of August 22 Ebonyi LG elections • Osun IPAC urges unity, swears in caretaker committee • FG fine on sponsor forced ‘Who Wants To Be A Millionaire’ off air — Frank Edoho • Oil firms making too much from Iran war – Trump • English FA to withdraw support for Infantino • Priscilla Ojo & Juma Jux Just Served the Sweetest Matching Traditional Wedding Looks • Delta unveils $100m fund to lure investors as FG backs diversification • NEC approves $4.5bn refinancing of $3.3bn oil-backed loan • 2027: Come, tell Nigerians primary, secondary school you attended – Kalu challenges Tinubu • LAFC co-managing owner Larry Berg voted as next MLS commissioner • Former deputy bureau chief of The Guardian, Anietie Akpan, dies • Nollywood Actress Maureen Okpoko opens up on battle with blindness [VIDEO] • Barca Need A Capable Striker –Flick • Igbo community group in Abuja cautions Southeast leaders against blanket endorsement of Tinubu • I used to borrow to maintain my lifestyle – Timini Egbuson • Arsenal weigh €150m summer move for Vinicius Junior • Okonjo-Iweala says Nigeria needs infrastructure maintenance, not just bigger budgets • Nigeria must deliver competitive barrels to win investment – Seplat’s CEO • NNPP drags INEC, seeks Abdulsalami committee’s intervention over candidates’ nomination • Africa and the imperatives of leadership, By Toyin Falola • APC kicks off campaign ahead of August 22 Ebonyi LG elections • Osun IPAC urges unity, swears in caretaker committee • FG fine on sponsor forced ‘Who Wants To Be A Millionaire’ off air — Frank Edoho • Oil firms making too much from Iran war – Trump • English FA to withdraw support for Infantino
Benki ya Capital One yaeleza sababu kufunga akaunti za Trump
Back to Home

Benki ya Capital One yaeleza sababu kufunga akaunti za Trump

Mwananchi about 3 hours 3 mins read
Dar es Salaam. Benki ya Capital One Financial imeieleza mahakama, uamuzi wake wa kufunga zaidi ya akaunti 300 zilizokuwa zinahusishwa na Kampuni ya Trump mwaka 2021 ulitokana na tathimini ya wataalamu wa kudhibiti utakatishaji fedha, ikipinga madai kuwa hatua hiyo ilichochewa na misimamo ya kisiasa. Katika nyaraka zilizowasilishwa mahakamani Ijumaa, Capital One imeomba kesi iliyofunguliwa dhidi yake itupiliwe mbali, ikieleza akaunti hizo hazikufungwa kwa misingi ya kisiasa au kidini, bali baada ya uchambuzi uliofanywa na kitengo chake cha kupambana na utakatishaji fedha (AML) kwa kuzingatia sera za benki na miongozo ya wasimamizi wa sekta ya fedha. Hii ni mara ya kwanza kwa benki kueleza rasmi mahakamani kuwa sababu za udhibiti wa utakatishaji fedha zilihusika katika uamuzi wa kufunga akaunti za biashara ya familia ya Rais wa Marekani, Donald Trump. Hata hivyo, Capital One imesisitiza kuwa haijawahi kuituhumu Kampuni ya Trump kujihusisha na utakatishaji fedha haramu, bali ilichukua hatua hiyo baada ya tathimini ya ndani kuhusu miamala iliyokuwa ikifanyika kwenye akaunti hizo. Benki hiyo ilitoa taarifa Machi, 2021 kuhusu mpango wake wa kufunga zaidi ya akaunti 300 zilizokuwa zinahusishwa na kampuni ya Trump (Trump Organization). Machi 2025, Trump Organization pamoja na Eric Trump, mtoto wa Trump, waliifungulia Capital One kesi katika Mahakama ya Shirikisho ya Florida wakidai benki hiyo ilifunga akaunti hizo kutokana na kile walichokiita msimamo wa kibaguzi ‘woke’ na kutaka kuendana na hali ya kisiasa iliyofuatia vurugu za Januari 6, 2021 katika jengo la Bunge la Marekani. Mahakama ya Shirikisho ya Miami tayari imeshatupilia mbali mara mbili malalamiko yaliyowasilishwa na walalamikaji, lakini kila mara imewapa nafasi ya kurekebisha na kuwasilisha upya hati ya madai. Capital One imeieleza mahakama kuwa hati mpya ya madai iliyowasilishwa Julai mwaka huu bado ina upungufu uleule uliokuwapo katika malalamiko yaliyotangulia. Aidha, benki hiyo imeeleza kuwa madai ya Trump Organization kwamba kufungwa kwa akaunti kulichochewa na sababu za kisiasa hayana msingi, ikidai yamejengwa juu ya nukuu zilizochaguliwa kwa upendeleo bila kuzingatia muktadha mzima wa nyaraka zilizowasilishwa mahakamani. Kwa mujibu wa Capital One, aina ya miamala iliyobainika kwenye akaunti hizo ni miongoni mwa shughuli ambazo miongozo ya mamlaka za fedha nchini Marekani, huzitambua kama zinazostahili kufanyiwa uchunguzi wa kina kwa madhumuni ya kudhibiti utakatishaji fedha. Kesi hiyo inaendelea wakati utawala wa Rais Donald Trump katika muhula wake wa pili ukiendelea kuishinikiza sekta ya benki, ukisisitiza madai ya wahafidhina kuwa baadhi ya taasisi kubwa za kifedha zimekuwa zikiwabagua wateja kutokana na misimamo yao ya kisiasa. Mwaka 2019, wakati wa muhula wake wa kwanza madarakani, Trump aliishtaki Capital One pamoja na Deutsche Bank akitaka kuzizuia benki hizo kutoa taarifa zake za kifedha kwa Bunge la Marekani, ambalo wakati huo lilikuwa linaendesha uchunguzi ulioongozwa na wabunge wa Chama cha Democratic. Habari hii imeandikwa kwa msaada wa Shirika la Habari la Reuters.

This article was sourced from an external publication.

Share this article
OneClick Africa Logo

Africa's premier digital hub for impactful news, entertainment, and business insights.

© 2026 OneClick Africa. All rights reserved.