Dodoma. Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) kimetangaza kuandaa maonyesho ya ajira na biashara, maarufu ‘Career Fair’ yatakayofanyika Mei 29 hadi 30, 2026, yakilenga kuwaunganisha vijana na fursa mbalimbali za ajira, mafunzo kwa vitendo pamoja na ujasiriamali.
Maonyesho hayo yatakayofanyika katika kampasi ya chuo hicho jijini Dar es Salaam yamebeba kaulimbiu isemayo, “Ubunifu na Ujuzi kwa Vijana, Msingi wa Ukuaji wa Biashara na Uchumi Tanzania.”
Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumamosi, Mei 23, 2026 jijini Dodoma, Mkuu wa chuo hicho, Profesa Edda Lwoga amesema maonyesho hayo yatafanyika kwa mara ya pili tangu kuanzishwa kwake mwaka jana, na tayari yameanza kuonyesha matokeo chanya kwa wanafunzi pamoja na vijana wanaotafuta ajira na fursa za kujiajiri.
“Lengo letu ni kuwaonyesha vijana fursa mbalimbali za ajira, ‘internship’ na biashara ili waweze kujiajiri na hata kuajiri wengine. Tunataka vijana watumie ubunifu wao kuleta suluhisho katika jamii na kukuza uchumi,” amesema Profesa Lwoga.
Kwa mujibu wa chuo hicho, taasisi mbalimbali za sekta binafsi na umma zinatarajiwa kushiriki katika maonesho hayo kwa kuwasilisha fursa za ajira, mafunzo kwa vitendo pamoja na huduma za kifedha.
Baadhi ya taasisi zilizotajwa kushiriki ni pamoja na benki ya CRDB, Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Tume ya Ushindani (FCC), Shirikisho la Wenye Viwanda Tanzania (CTI) na Chama cha Wanawake Wafanyabiashara Tanzania (TWCCIA).
Aidha, wanafunzi wa CBE, wahitimu wa zamani na vijana kutoka taasisi mbalimbali watapata nafasi ya kuonesha bidhaa, mifumo na ubunifu waliyoibuni, huku shule za sekondari kutoka Dar es Salaam nazo zikitarajiwa kushiriki kuonyesha kazi za wanafunzi wao.
Profesa Lwoga amesema CBE imeendelea kupanua uwezo wake wa kutoa elimu ya biashara nchini, ambapo idadi ya wanafunzi imeongezeka kutoka takribani 12,977 mwaka 2021 hadi kufikia wanafunzi 24,026 mwaka 2026 katika kampasi za Dar es Salaam, Dodoma, Mwanza na Mbeya ndani ya kipindi cha miaka mitano iliyopita.
Amesema sambamba na ongezeko hilo, chuo hicho pia kimeongeza programu za masomo kutoka 63 hadi 71 ili kuendana na mahitaji ya soko la ajira na mabadiliko ya teknolojia.
Wakati huohuo, Mkurugenzi wa CBE Kampasi ya Dodoma, Dk Josephine Churk amesema kampasi hiyo imeendelea kuwaibua vijana wabunifu kupitia programu ya kuatamia kazi za wanafunzi, huku baadhi yao wakifanikiwa kubuni mifumo ya kidijitali inayotatua changamoto mbalimbali katika jamii.
Dk Churk amesema baadhi ya vijana wamebuni mifumo inayounganisha huduma mbalimbali zinazotumiwa na wanafunzi wa vyuo vikuu ikiwamo mifumo ya TCU, usajili wa vyuo na mikopo ya elimu ya juu.
“Ubunifu wao ulitambuliwa hadi na Google na sasa wanajipatia kipato huku wengine wakiajiri wenzao,” amesema Dk Churk
Amesema wengine wamebuni mifumo ya kuukata tiketi za mabasi, kuunganisha wakulima na masoko, pamoja na mifumo ya ukusanyaji taka majumbani inayowawezesha wananchi kuwasiliana moja kwa moja na watoa huduma kupitia teknolojia ya kidijitali.
“Tunao vijana wanaobuni suluhisho za changamoto za kila siku katika jamii kupitia teknolojia. Tunaamini kupitia Career Fair vijana wengi zaidi watahamasika kutumia ubunifu wao kujiajiri,” amesema.

DR Congo
View AllSenegal
View All
Senegal | 3h ago Faye, Senegal President sacks PM, dissolves cabinet amid deepening crisis
Business Day

Senegal | 5h ago Senegal’s President sacks PM, dissolves government after months of tension
Premium TImes

Senegal | 5h ago Senegal’s president sacks PM after months of tensions
Vanguard Nigeria

Senegal | 6h ago Senegal President Faye sacks Prime Minister Sonko, ministers
Daily Post
ECOWAS
View All AD

This Day
Punch Nigeria