TRENDING
Chongolo: Wauzaji pembejeo feki hawana tofauti na wauaji
Back to Home

Chongolo: Wauzaji pembejeo feki hawana tofauti na wauaji

Mwananchi about 2 hours 3 mins read
Songwe. Wafanyabiashara wanaouza pembejeo feki na wanaojihusisha na utoroshaji wa mbolea ya ruzuku kwenda nchi jirani wamepewa onyo na Waziri wa Kilimo, Daniel Chongolo huku akiwafananisha na wauaji kutokana na madhara wanayosababisha kwa wakulima na Taifa kwa jumla. Chongolo amesema vitendo hivyo ni hujuma kubwa inayoweza kuathiri uzalishaji wa chakula, usalama wa chakula nchini na kuwakosesha wakulima haki ya kupata pembejeo bora kwa ajili ya kuongeza uzalishaji. Akizungumza na wafanyabiashara wa pembejeo za kilimo na mifugo mkoani Songwe jana Ijumaa Julai 10, 2026 amesema Serikali haitakuwa na huruma kwa watu watakaobainika kuuza pembejeo zisizokidhi viwango, kuficha au kutorosha mbolea ya ruzuku pamoja na kupandisha bei kiholela. Amesema wafanyabiashara watakaokiuka sheria watafutiwa leseni na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria ili kulinda masilahi ya wakulima na fedha zinazotumika katika mpango wa ruzuku ya mbolea. “Watu wanaouza pembejeo feki na wanaotorosha mbolea ya ruzuku hawana tofauti na wauaji, kwa sababu wanawaangusha wakulima, wanahatarisha uzalishaji wa chakula na kuathiri uchumi wa nchi,” amesema Chongolo. Amesema Serikali inawekeza fedha nyingi katika sekta ya kilimo kupitia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 na Agenda 10/30, hivyo ni lazima kila shilingi inayowekwa iwe na manufaa kwa mkulima. “Fedha zinazowekezwa na Serikali kwenye ruzuku ya mbolea lazima ziwafikie walengwa na ziongeze uzalishaji wa mazao nchini,” amesema. Hata hivyo, Chongolo amewahakikishia wakulima kuwa hakuna upungufu wa mbolea nchini, akisema kwa sasa kuna tani 248,617 za aina mbalimbali zilizopo tayari. Amesema tani nyingine 313,800 zinatarajiwa kuingia nchini kati ya Julai na Septemba mwaka huu ili kuongeza upatikanaji wa pembejeo hiyo. “Niwasisitizie wakulima kuwa hakuna upungufu wa mbolea nchini. Serikali kupitia Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) imelenga kuhakikisha tani milioni 1.5 za mbolea zinapatikana katika mwaka wa fedha 2026/27 ili kukidhi mahitaji ya wakulima wote,” amesema. Amewataka wafanyabiashara wa pembejeo kufanya biashara kwa kuzingatia sheria, kuuza bidhaa kwa bei elekezi, kutunza kumbukumbu sahihi na kuhakikisha wanawafikia wakulima wanaostahili. Mbunge wa Mbozi, Onesmo Mkondya ameeleza changamoto ya upatikanaji wa mbolea ya ruzuku katika Mkoa wa Songwe, akisema hadi sasa kuna kampuni moja inayodaiwa kuingiza mbolea hiyo mkoani humo. Amesema hali hiyo imeibua hofu kwa wakulima na kuiomba Serikali kuongeza idadi ya kampuni zinazoruhusiwa kusambaza mbolea ili kuongeza upatikanaji wake. “Licha ya Serikali kutangaza uwepo wa mbolea ya ruzuku, bado kuna changamoto kubwa ya upatikanaji wake. Tunaomba Serikali itoe vibali kwa kampuni nyingi ili wananchi wapate mbolea kwa wingi ndani ya Mkoa wa Songwe,” amesema Mkondya. Mbunge wa Vwawa, Japhet Hasunga amesema tatizo la pembejeo na mbegu feki limeendelea kuwa changamoto kubwa kwa wakulima na kuitaka Serikali kuchukua hatua kali zaidi dhidi ya wahusika. Mwenyekiti wa Umoja wa Wafanyabiashara wa Pembejeo, Boniface Masika ameiomba Serikali kuzuia kampuni za mbolea kuuza moja kwa moja kwa wakulima badala yake zitumie mfumo wa mawakala ili kulinda biashara ya wafanyabiashara waliopo kwenye mfumo wa usambazaji. Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Jabiri Omari Makame amesema mkoa huo umejipanga kudhibiti vitendo vyote vya hujuma vinavyohusiana na pembejeo za kilimo. “Ni kuhakikisha tunapambana na wauzaji wa pembejeo feki na watoroshaji ili kuwalinda wakulima wa Mkoa wa Songwe ambao wanategemea kilimo kama chanzo kikuu cha kipato,” amesema Makame.

This article was sourced from an external publication.

Share this article

Comments (0)

Want to join the discussion?

Sign in to post comments and engage with the community.

Be the first to comment!

DR Congo

View All

Senegal

View All
AD

Traditional Affairs

View All

Somalia

View All
AD
OneClick Africa Logo

Africa's premier digital hub for impactful news, entertainment, and business insights.

© 2026 OneClick Africa. All rights reserved.