TRENDING
‘Toyin Abraham didn’t destroy my marriage’ — Femi Adebayo’s ex-wife clarifies • ADC demands probe of INEC, Lagos CP over pro-Tinubu activities • Sera mpya ya sayansi, teknolojia itakavyowasaidia wabunifu nchini • ‘Dangerous gamble’ – Nnamdi Kanu’s lawyer warns against prosecuting Sowore close to 2027 polls • Rashford not leaving Man United – Fabrizio Romano • Brazil to face India for first time in October 3 friendly • NFF Reschedules Elective Congress For September 27 • Cherubim & Seraphim’s Spiritual Father Emmanuel Alogbo dies at 93 • N400bn needed to complete Millennium Tower — Wike • State electricity markets risk losing investors without harmonised regulations – FCCPC • Oyo Sets Up Judicial Commission of Inquiry Over Oriire Abduction • Messi Returns To Miami Training After World Cup Break • Kogi Moves To Curb Human Trafficking, Warns Against Online Recruitment Scams • NDLEA Raises Alarm Over Rising Involvement Of Women In Drug Trafficking In Edo • We’re Dying Of Hunger, Naridom Community Cries Out After Bandits Raze Food Shops • Judge Escapes Through Window As Bandits Attack Court In Katsina • LPDC suspends senior lawyer Gadzama from legal practice for three years • Reps probe prolonged Bille gas leak, demand urgent action as emissions persist • Court remands four over $5.29m fraud in Lagos • Osun election: Political parties sign accord for peaceful poll • ‘Toyin Abraham didn’t destroy my marriage’ — Femi Adebayo’s ex-wife clarifies • ADC demands probe of INEC, Lagos CP over pro-Tinubu activities • Sera mpya ya sayansi, teknolojia itakavyowasaidia wabunifu nchini • ‘Dangerous gamble’ – Nnamdi Kanu’s lawyer warns against prosecuting Sowore close to 2027 polls • Rashford not leaving Man United – Fabrizio Romano • Brazil to face India for first time in October 3 friendly • NFF Reschedules Elective Congress For September 27 • Cherubim & Seraphim’s Spiritual Father Emmanuel Alogbo dies at 93 • N400bn needed to complete Millennium Tower — Wike • State electricity markets risk losing investors without harmonised regulations – FCCPC • Oyo Sets Up Judicial Commission of Inquiry Over Oriire Abduction • Messi Returns To Miami Training After World Cup Break • Kogi Moves To Curb Human Trafficking, Warns Against Online Recruitment Scams • NDLEA Raises Alarm Over Rising Involvement Of Women In Drug Trafficking In Edo • We’re Dying Of Hunger, Naridom Community Cries Out After Bandits Raze Food Shops • Judge Escapes Through Window As Bandits Attack Court In Katsina • LPDC suspends senior lawyer Gadzama from legal practice for three years • Reps probe prolonged Bille gas leak, demand urgent action as emissions persist • Court remands four over $5.29m fraud in Lagos • Osun election: Political parties sign accord for peaceful poll
Dk Besigye alivyoanguka mahakamani akigomea mawakili wa Serikali
Back to Home

Dk Besigye alivyoanguka mahakamani akigomea mawakili wa Serikali

Mwananchi about 3 hours 4 mins read
Kampala. Kiongozi mkongwe wa upinzani nchini Uganda na mwanzilishi wa chama cha Forum for Democratic Change (FDC), Dk Kizza Besigye, ameanguka na kupoteza fahamu akiwa ndani ya Mahakama Kuu akipinga kuwakilishwa na mawakili walioteuliwa na Serikali katika kesi ya uhaini inayomkabili. Besigye (70) alisisitiza kuwa anapaswa kutetewa na mawakili aliowachagua, huku akieleza kuwa haki hiyo imekiukwa baada ya wakili wake mkuu kukamatwa mwezi uliopita na kushtakiwa kwa madai ya kushindwa kutoa taarifa kuhusu vitendo vinavyohusiana na uhaini. Mashuhuda waliokuwapo mahakamani walisema mwanasiasa huyo alisikika akipaza sauti mara kadhaa akisema, “Stop! Stop! Stop!” (kwa maana ya simamisha, simamisha, simamisha), kabla ya kuanguka ndani ya kizimba cha washtakiwa. Askari magereza na wahudumu wa afya walimkimbilia na kumtoa nje ya ukumbi wa mahakama kwa matibabu ya dharura kabla ya kukimbizwa hospitalini jijini Kampala, ambako amelazwa katika Chumba cha Uangalizi Maalumu (ICU). Mke wake, Winnie Byanyima, amesema Dk Besigye alipoteza fahamu, hakuwa akizungumza wala kuitikia maumivu, hali iliyoibua hofu kuhusu afya yake na kuongeza mjadala kuhusu mwenendo wa kesi hiyo yenye mvuto mkubwa wa kisiasa. Dk Besigye, aliyewahi kugombea urais mara nne dhidi ya Rais Yoweri Museveni, alianguka Jumatano, Julai 29, 2026, baada ya kupinga uamuzi wa mahakama kuendelea na usikilizwaji wa kesi huku akidai amenyimwa haki ya kutetewa na mawakili aliowachagua. Alazwa ICU, mkewe atoa taarifa Baada ya tukio hilo, Dk Besigye aliwahishwa katika hospitali moja jijini Kampala, ambako amelazwa ICU. Mke wake, Winnie Byanyima, ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kupambana na Ukimwi (UNAIDS), amesema kupitia mtandao wa X kuwa mume wake alikuwa amepoteza fahamu na hali yake ilikuwa mbaya. Kwa mujibu wa Byanyima, Besigye alikuwa “hapotezi tu fahamu, bali pia hakuwa akizungumza wala kuitikia hata maumivu”, hali iliyoongeza hofu kuhusu afya yake. Akipinga mawakili wa Serikali Taarifa zimeeleza kuwa kabla ya kuanguka, Besigye alikuwa akipinga hatua ya upande wa mashtaka na mahakama kuruhusu mawakili walioteuliwa na Serikali kumwakilisha badala ya mawakili wake aliowachagua. Mawakili wa utetezi wa Besigye wamekuwa wakikumbwa na changamoto mbalimbali. Wakili wake mkuu alikamatwa mwezi uliopita na kufunguliwa mashtaka kwa madai ya kushindwa kutoa taarifa kuhusu vitendo vinavyohusiana na uhaini, jambo ambalo limeifanya timu yake ya utetezi kudhoofika. Amekuwa rumande tangu Novemba 2024 Dk Besigye anashikiliwa tangu Novemba 2024 baada ya kukamatwa kutokana na mazingira yaliyoibua mjadala mkubwa ndani na nje ya Uganda. Kwa mujibu wa taarifa mbalimbali, Besigye alikuwa amesafiri kutoka Entebbe kwenda Nairobi, Kenya, kwa shughuli binafsi. Inadaiwa kuwa alipofika Nairobi alikutana na watu waliodhaniwa kuwa maofisa wa usalama wa Kenya, kabla ya kutoweka na baadaye kujitokeza akiwa chini ya ulinzi wa mamlaka za Uganda. Tukio hilo lilizua lawama na maswali kuhusu uwezekano wa kuwapo kwa ushirikiano wa kiintelijensia kati ya Kenya na Uganda. Serikali ya Kenya ilikanusha kuhusika katika kukamatwa kwake na kusema ilianza uchunguzi wa tukio hilo, huku Serikali ya Uganda ikisisitiza kuwa Kenya ilikuwa na taarifa kuhusu operesheni hiyo kupitia mawasiliano ya kiusalama kati ya nchi hizo mbili. Mahakama yaweka masharti mapya Wakati huo huo, Mahakama ya Uganda imeanzisha mwongozo mpya wa uendeshaji wa kesi zenye maslahi makubwa kwa umma. Masharti hayo yanajumuisha kupunguza idadi ya watu wanaoruhusiwa kuingia mahakamani, kupiga marufuku upigaji picha, matangazo ya moja kwa moja (live streaming), pamoja na matumizi ya vifaa vya kielektroniki ndani ya ukumbi wa mahakama. Hatua hiyo imeibua mjadala kuhusu uwazi wa mwenendo wa kesi zinazohusisha wanasiasa wa upinzani. Historia yake Dk Besigye ni mmoja wa wanasiasa mashuhuri zaidi wa upinzani nchini Uganda na mwanzilishi wa chama cha Forum for Democratic Change (FDC), ambacho kwa miaka mingi kilikuwa chama kikuu cha upinzani nchini humo. Katika miaka ya karibuni, nafasi hiyo imechukuliwa na National Unity Platform (NUP), kinachoongozwa na mwanasiasa na msanii Robert Kyagulanyi, maarufu Bobi Wine, baada ya chama hicho kupata mafanikio makubwa katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2021. Dk Besigye amebaki kuwa mmoja wa sauti zenye ushawishi mkubwa katika siasa za upinzani nchini Uganda, licha ya kutoshika nafasi ya uongozi ndani ya FDC kwa sasa. Pia, aliwahi kuwa daktari wa Rais Yoweri Museveni wakati wa vita vya msituni vilivyomwingiza madarakani mwaka 1986. Baadaye aligeuka kuwa mkosoaji mkubwa wa Serikali ya Museveni na akagombea urais mara nne dhidi yake katika uchaguzi wa mwaka 2001, 2006, 2011 na 2016, lakini hakuwahi kushinda. Hakugombea uchaguzi mkuu wa mwaka 2021, ingawa aliendelea kuwa mmoja wa sauti muhimu za upinzani nchini humo.

This article was sourced from an external publication.

Share this article
OneClick Africa Logo

Africa's premier digital hub for impactful news, entertainment, and business insights.

© 2026 OneClick Africa. All rights reserved.