TRENDING
Propaganda has expiry date — PDP blasts Makinde over Ibadan meeting • Mahama to chair special cabinet meeting on implementation of constitutional review proposals today • China and US should be partners, not rivals — Xi Jinping tells Trump • HIV positive father remanded for allegedly raping, infecting daughter • MSD, hospitali watafuta suluhisho la madeni • Analysts see April inflation rise strengthening case for CBN rate hold • Tier-1 banks grow deposits to N114trn as lending slows • Africa turns to Luanda for talks on growth financing, economic resilience • ‘It’s Scary’ — Iheanacho Reacts To Late Penalty Winner Against Motherwell • تحول ميداني لافت في النيل الأزرق بعد سيطرة قوات “تأسيس” على مقجة • Sand, Pinstripes, and Peacock Feathers: Tyla’s Met Gala Journey So Far • EOCO detains wife of Dr. Sledge • Angry youth hunt alleged sex predator in Heman • Court jails “okadaman” 8 years for robbery • CTVET to begin first harmonised certificate II and traditional TVET examination on May 18 • Trust hospital midwife arrested for alleged child trafficking • BREAKING: 2027: Former Ondo Governor, Mimiko officially joins APC • 2027: Plateau PDP screens 131 Assembly, three Senatorial aspirants • Benue LG workers begin two-week strike over unpaid salaries • FULL LIST: Top 10 best goalkeepers in Europe’s clean sheet rankings • Propaganda has expiry date — PDP blasts Makinde over Ibadan meeting • Mahama to chair special cabinet meeting on implementation of constitutional review proposals today • China and US should be partners, not rivals — Xi Jinping tells Trump • HIV positive father remanded for allegedly raping, infecting daughter • MSD, hospitali watafuta suluhisho la madeni • Analysts see April inflation rise strengthening case for CBN rate hold • Tier-1 banks grow deposits to N114trn as lending slows • Africa turns to Luanda for talks on growth financing, economic resilience • ‘It’s Scary’ — Iheanacho Reacts To Late Penalty Winner Against Motherwell • تحول ميداني لافت في النيل الأزرق بعد سيطرة قوات “تأسيس” على مقجة • Sand, Pinstripes, and Peacock Feathers: Tyla’s Met Gala Journey So Far • EOCO detains wife of Dr. Sledge • Angry youth hunt alleged sex predator in Heman • Court jails “okadaman” 8 years for robbery • CTVET to begin first harmonised certificate II and traditional TVET examination on May 18 • Trust hospital midwife arrested for alleged child trafficking • BREAKING: 2027: Former Ondo Governor, Mimiko officially joins APC • 2027: Plateau PDP screens 131 Assembly, three Senatorial aspirants • Benue LG workers begin two-week strike over unpaid salaries • FULL LIST: Top 10 best goalkeepers in Europe’s clean sheet rankings
Drones zitakavyotumika kutokomeza malaria Zanzibar
Back to Home

Drones zitakavyotumika kutokomeza malaria Zanzibar

Mwananchi about 2 hours 4 mins read
Unguja. Katika kuhakikisha Zanzibar inafikia lengo la kutokomeza malaria kabisa, mradi maalumu wa matumizi ya ndege zisizo na rubani (drones) kwa ajili ya kutambua na kuangamiza mazalia ya mbu, umezinduliwa rasmi. Mradi huo unaojulikana kama Teknolojia Mahiri ya Drones kwa Zanzibar Isiyo na Malaria, unatekelezwa kwa ushirikiano kati ya Wizara ya Afya Zanzibar kupitia Mpango wa Zanzibar wa Kutokomeza Malaria (ZAMEP), Shirika la Afya Duniani (WHO), Kampuni ya Sora Technology kutoka Japan pamoja na Taasisi ya Afya ya Ifakara (IHI). Mradi huo unafadhiliwa na Serikali ya Japan kwa gharama ya Sh1 bilioni. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi huo leo Jumatano, Mei 13, 2026, Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Zanzibar, Dk Miraji Mngereza Mzee amesema huu ni mradi wa kwanza Zanzibar unaounganisha matumizi ya teknolojia ya kisasa na ushirikishwaji wa jamii katika mapambano dhidi ya malaria. Amesema kwa miaka mingi Zanzibar imekuwa ikikabiliwa na changamoto ya malaria, lakini kwa sasa kiwango cha maambukizi kimepungua hadi chini ya asilimia moja. Amesema matumizi ya teknolojia hiyo pamoja na ushirikiano wa wananchi, utaisaidia Zanzibar kuandika historia mpya ya kutokuwa na malaria. “Zanzibar inapaswa kuwa huru dhidi ya malaria na kutambuliwa duniani kama eneo lisilo na maambukizi ya ugonjwa huo,” amesema Dk Mngereza. Amefafanua matumizi ya drones yatawezesha kufikiwa kwa maeneo ambayo ni magumu kuyafikia kwa njia za kawaida. Aidha, teknolojia hiyo itarahisisha kuangamiza mazalia ya mbu kwa haraka zaidi tofauti na mfumo wa kawaida unaoweza kuchukua hadi siku tatu. Naye Mkurugenzi wa Kinga na Elimu ya Afya kutoka Wizara ya Afya Zanzibar, Dk Salim Slim, amesema mradi huo unatarajiwa kuleta mabadiliko makubwa kwenye juhudi za kutokomeza malaria visiwani humo. Amesema kiwango cha maambukizi ya malaria Zanzibar kwa sasa kimefikia asilimia 0.04 na kinaendelea kupungua kwa kasi. “Kuna maeneo ambayo binadamu hawezi kuyafikia kwa urahisi, hivyo kwa kutumia ndege nyuki tutafika maeneo mengi zaidi. Drones hizi zitakuwa na uwezo wa kubeba dawa na kunyunyizia katika maeneo mbalimbali, jambo litakalopunguza gharama za kutumia njia za kawaida,” amesema Dk Slim. Hata hivyo, ameonya licha ya mafanikio yaliyopo, malaria bado ipo na inaendelea kusababisha vifo. Amesema takwimu zinaonyesha kuwa vijana wenye umri kati ya miaka 15 hadi 40 wako katika hatari zaidi ya kuambukizwa malaria kutokana na tabia ya kukaa nje usiku na kujikusanya katika maeneo mbalimbali. Aidha, amesema upande wa Pemba wanatarajia kufikia hatua ya kutokuwa na malaria ifikapo mwanzoni mwa mwaka 2027, huku akisisitiza umuhimu wa kuendelea kudhibiti mazalia ya mbu ili kuzuia ugonjwa huo kurejea tena. Kwa upande wake, mwakilishi kutoka ubalozi wa Japan, Jin Hashimoto, amesema Serikali ya nchi hiyo itaendelea kusaidia kukabiliana na changamoto mbalimbali za kijamii kupitia matumizi ya teknolojia, ubunifu na utaalamu wa kisasa. Amesema wanaamini matumizi ya teknolojia ya drones yatasaidia kupunguza mazalia ya mbu na kuimarisha udhibiti wa malaria Zanzibar. “Tunaamini mradi huu pia utasaidia kupatikana kwa takwimu sahihi na zenye ushahidi kuhusu malaria nchini. Sekta ya afya inaendelea kuwa miongoni mwa maeneo ya kipaumbele kwa serikali ya Japan,” amesema Hashimoto. Naye Mkuu wa Ofisi ya Uhusiano ya WHO Zanzibar, Dk Ndoungou Salla amesema Wizara ya Afya kupitia ZAMEP itatoa uongozi wa kimkakati, uratibu wa kisheria pamoja na usimamizi wa utekelezaji wa mradi huo ili kuhakikisha matumizi ya drones yanaingizwa rasmi katika mifumo ya kitaifa ya kudhibiti malaria. Amesema WHO itaendelea kutoa mwongozo wa kitaalamu na kuhakikisha ushirikiano mzuri baina ya wadau wote wanaotekeleza mradi huo. Amefafanua kuwa kampuni ya Sora Technology itahusika na usambazaji wa mifumo ya drones sambamba na kusaidia kujenga uwezo wa ndani katika matumizi ya teknolojia hiyo kwa kuzingatia takwimu na ushahidi wa kisayansi. “Tunapongeza Serikali ya Zanzibar kupitia ZAMEP kwa uongozi wake imara na dhamira ya dhati ya kutokomeza malaria. Mafanikio ya Zanzibar ya kudumisha kiwango cha maambukizi chini ya asilimia moja yanaonyesha umuhimu wa uwekezaji, ushirikiano na ubunifu endelevu,” amesema Dk Salla. Mradi huo unatarajiwa kutumia teknolojia ya drones pamoja na akili bandia (AI) katika kuboresha utambuzi na usimamizi wa maeneo yanayotumika kama mazalia ya mbu. Ubunifu huo utahusisha upigaji picha na ramani za anga za maeneo yenye mazalia ya viwavi wa mbu, ufuatiliaji wa aina za mbu wanaosambaza malaria, pamoja na matumizi ya ramani za utabiri zitakazosaidia kuelekeza kwa usahihi maeneo yatakayonyunyiziwa dawa za kuua viwavi.

This article was sourced from an external publication.

Share this article

Comments (0)

Want to join the discussion?

Sign in to post comments and engage with the community.

Be the first to comment!

Traditional Affairs

View All

Somalia

View All
AD