Dodoma. Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi amemwelekeza Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) kusitisha utoaji wa vibali vya mikutano ya hadhara kwa vyama vyote vya siasa kwa kipindi hiki, akieleza kuwa hatua hiyo inalenga kuimarisha usalama na kudhibiti vitendo vya uhalifu vinavyoweza kujitokeza.
Akijibu maswali ya wabunge bungeni jijini Dodoma leo, Juni 26, Katambi amesema serikali imebaini uwepo wa matishio ya kiusalama, ikiwemo watu wanaodaiwa kukamatwa wakiwa na silaha, mafuta ya petroli na wakipanga vitendo vya uhalifu, hivyo vyombo vya ulinzi na usalama vimepewa maelekezo ya kuongeza ulinzi katika maeneo yenye viashiria vya hatari.
Pia, amewaagiza wakuu wa mikoa na wilaya kuimarisha usimamizi wa kamati za ulinzi na usalama katika maeneo yao, huku akiliagiza Jeshi la Polisi kuchukua hatua dhidi ya maeneo ya biashara yanayokiuka sheria au yanayohatarisha usalama, ikiwemo kuyafungia kwa muda pale itakapobidi.
Katambi amewataka pia wamiliki wa hoteli, nyumba za wageni, Airbnb na loji kote nchini kuhakikisha wageni wote wanaosajiliwa wanatumia vitambulisho vya Nida, akionya kuwa hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi ya wamiliki watakaokiuka maelekezo hayo.

Agriculture
View All
Food & Nutrition | 22m ago Read food labels before purchase, consumption – NAFDAC DG urges Nigerians
Daily Post

Food & Nutrition | 52m ago Read food labels before buying packaged foods, NAFDAC tells Nigerians
Punch Nigeria

Food & Nutrition | 1h ago Serikali yasitisha mikutano ya hadhara vyama vya siasa Tanzania
Mwananchi

Food & Nutrition | 1h ago Serikali yasitisha mikutano ya hadhara vyama vya siasa
Mwananchi
