TRENDING
SpaceX's Starship splashes down in Indian Ocean after successful test flight • ECOWAS orders release of detained Nigerian onion trucks • Insecurity: Tinubu charges Nigerian universities for evidence-based solutions • Chanjo, uchunguzi wa homa ya ini kutolewa bure Muhimbili • Group Calls For Immediate Rescue Of Over 170 Abductees In Kwara Communities • ‘I may be arrested for speaking truth’ – Al-Mustapha • Gumi questions absence of government dialogue with Boko Haram, bandits • Stop Politicising National Security, Allow Gen Musa to Continue His Work, Says Darazo • Two Policemen, Vigilante Killed As Terrorists Abduct Zamfara LG Chairman • Police investigate as unidentified pusher dies in wheelbarrow during nap • Manufacturers cite power, costly credit, logistics as key competitiveness constraints • CBN seen holding rates through 2026 • Mchengerwa awataka viongozi kushuka kwa wananchi kutatua kero • Bus preaching distracts drivers, can lead to breach of peace – MURIC backs FRSC bill • Sirro atoa neno kwa washiriki wa Nane Nane • Ndume backs army expansion, calls for more equipment, better welfare • 2027: Peter Obi remains best choice to rebuild Nigeria  — PDP chieftain • I’m not opposed to Tinubu’s second-term bid — Otti • Kebbi rejects allegations of abandoning communities to bandits • Kusambaa mashambulizi ya Iran kwazua hofu Mashariki ya Kati • SpaceX's Starship splashes down in Indian Ocean after successful test flight • ECOWAS orders release of detained Nigerian onion trucks • Insecurity: Tinubu charges Nigerian universities for evidence-based solutions • Chanjo, uchunguzi wa homa ya ini kutolewa bure Muhimbili • Group Calls For Immediate Rescue Of Over 170 Abductees In Kwara Communities • ‘I may be arrested for speaking truth’ – Al-Mustapha • Gumi questions absence of government dialogue with Boko Haram, bandits • Stop Politicising National Security, Allow Gen Musa to Continue His Work, Says Darazo • Two Policemen, Vigilante Killed As Terrorists Abduct Zamfara LG Chairman • Police investigate as unidentified pusher dies in wheelbarrow during nap • Manufacturers cite power, costly credit, logistics as key competitiveness constraints • CBN seen holding rates through 2026 • Mchengerwa awataka viongozi kushuka kwa wananchi kutatua kero • Bus preaching distracts drivers, can lead to breach of peace – MURIC backs FRSC bill • Sirro atoa neno kwa washiriki wa Nane Nane • Ndume backs army expansion, calls for more equipment, better welfare • 2027: Peter Obi remains best choice to rebuild Nigeria  — PDP chieftain • I’m not opposed to Tinubu’s second-term bid — Otti • Kebbi rejects allegations of abandoning communities to bandits • Kusambaa mashambulizi ya Iran kwazua hofu Mashariki ya Kati
Serikali kubeba gharama mazishi ya watano wa familia moja waliozama bwawani
Back to Home

Serikali kubeba gharama mazishi ya watano wa familia moja waliozama bwawani

Mwananchi about 3 hours 3 mins read
Moshi. Serikali imeahidi kugharamia majeneza na usafiri wa mazishi ya watu watano wa familia moja waliopoteza maisha baada ya mtumbwi waliokuwa wakisafiria kupinduka katika Bwawa la Nyumba ya Mungu, Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro. Ahadi hiyo imetolewa leo na Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Godfrey Mnzava, alipofika kutoa pole kwa familia ya wafiwa katika Kijiji cha Chemchemi kilichopo Kata ya Arusha Chini. Ajali hiyo ilitokea Julai 23, 2026, wakati waumini wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG) Kijiji cha Chemchemi walipokuwa wakielekea kanisani katika Kitongoji cha Mikocheni ‘B’ kuhudhuria kongamano la Idara ya Wanawake. Katika ajali hiyo, wanawake wawili na watoto watatu wa familia moja walipoteza maisha huku watu wanane wakinusurika. Waliofariki dunia wametajwa kuwa ni Maria Andrea, Yustina Lazaro, Raima Andrea, Happy Andrea na Kelvini Andrea. Akizungumza na familia hiyo, Mnzava amesema Serikali imeguswa na msiba huo na imeamua kupokea maombi ya familia ya kupata msaada wa maandalizi ya mazishi yanayotarajiwa kufanyika Jumatatu, Julai 27, 2026. “Tumelichukua hilo na tutalifanyia kazi. Serikali itaandaa usafiri, lakini pia itabeba gharama za majeneza yote matano kama sehemu ya faraja na namna tulivyoguswa na msiba huu uliowakuta,” amesema Mnzava. Pamoja na kutoa pole, Mnzava ametumia fursa hiyo kuwatahadharisha wananchi wanaoishi na kufanya shughuli zao kandokando ya Bwawa la Nyumba ya Mungu kuchukua tahadhari kutokana na hali ya hewa kutokuwa salama. Amesema Mamlaka ya Hali ya Hewa na uongozi wa eneo hilo umekuwa ukitahadharisha mara kwa mara kuhusu upepo mkali na kuongezeka kwa kina cha maji. “Wananchi wanapaswa kuepuka shughuli zisizo za lazima bwawani kwa kipindi hiki, na wavuvi pia wanatakiwa kuzingatia kanuni na tahadhari zote wanapokuwa majini,” amesisitiza. Kwa upande wake, Mbunge wa Moshi Vijijini, Morris Makoi, aliyefika eneo hilo kuungana na Serikali, amesema msiba huo umeumiza jamii nzima kutokana na waliofariki kuwa katika safari ya kiimani. Makoi amechangia vyakula na vinywaji ikiwamo katoni 50 za maji, lita 20 za mafuta ya kupikia, kilo 50 za mchele na kreti 20 za soda, huku diwani wa eneo hilo,Leonard Waziri akichangia kilo 30 za mchele kusaidia msiba huo. Kwa niaba ya wafiwa na wanakijiji, mzee Lawrence Ngonyani ambaye amepoteza mwali na wajukuu watatu, ameishukuru Serikali, wananchi na viongozi wa jimbo hilo kwa kujitokeza kwa pamoja kuwafariji. “Sijawahi kuona Mkuu wa Wilaya, Mbunge na Mkurugenzi wakifuatana kwa pamoja kuja kutoa pole kijijini kwetu. Hili ni tukio la kwanza na limetupa faraja kubwa sana katika kipindi hiki kigumu,” amesema Ngonyani. Miili ya marehemu kwa sasa imehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mawenzi mjini Moshi.

This article was sourced from an external publication.

Share this article

Comments (0)

Want to join the discussion?

Sign in to post comments and engage with the community.

Be the first to comment!

Cameroon

View All

Senegal

View All
AD

DR Congo

View All

Traditional Affairs

View All
AD
OneClick Africa Logo

Africa's premier digital hub for impactful news, entertainment, and business insights.

© 2026 OneClick Africa. All rights reserved.