TRENDING
Man City still dream of Premier League glory after FA Cup win – Silva • Israel explores future without US military aid dependence • Yahaya hails peaceful Gombe APC primaries • Wauguzi Ludewa waonya kuomba uhamisho mara kwa mara • Sababu waishio mijini wanatajwa kuwa hatarini kwa shinikizo la damu • Manchester City win FA Cup final as Semenyo’s moment of magic floors Chelsea • Oyo school abduction: Kidnappers trapped in national park — Commissioner • Ujumbe wa Trump watupa zawadi ulizopewa China, kabla ya kupanda ndege • Wadau wataja mambo yatakayolikwamua Taifa • Dk Mwigulu aagiza mfanyabiashara arudishiwe vitu vyake • Presidency Affirms Al-Manuki’s Killing, Says 2024 Report Was A Case Of Mistaken Identity • FA Cup final player ratings: Chelsea 0-1 Manchester City • Guardiola makes history as Manchester City lift FA Cup • “Nigerians Now Teat Insecurity, Killings As Normal” – Jonathan • Students’ Abduction: We’re working with security agencies, says Makinde • Police arrest 10 over violence at Lagos APC primaries • Lagos Sanctions 15 Online Money Lending Firms Over Operational Violations • 2027: Don’t Stake Your Children’s School Fees on Primaries, Uzodimma Tells Imo APC Aspirants • Nigerian Navy Uncovers, Dismantles Illegal Refined Petroleum Products Depot in Rivers • Ex-Kwara Gov’s Aide, Ajakaye, Wins APC Federal Constituency Ticket • Man City still dream of Premier League glory after FA Cup win – Silva • Israel explores future without US military aid dependence • Yahaya hails peaceful Gombe APC primaries • Wauguzi Ludewa waonya kuomba uhamisho mara kwa mara • Sababu waishio mijini wanatajwa kuwa hatarini kwa shinikizo la damu • Manchester City win FA Cup final as Semenyo’s moment of magic floors Chelsea • Oyo school abduction: Kidnappers trapped in national park — Commissioner • Ujumbe wa Trump watupa zawadi ulizopewa China, kabla ya kupanda ndege • Wadau wataja mambo yatakayolikwamua Taifa • Dk Mwigulu aagiza mfanyabiashara arudishiwe vitu vyake • Presidency Affirms Al-Manuki’s Killing, Says 2024 Report Was A Case Of Mistaken Identity • FA Cup final player ratings: Chelsea 0-1 Manchester City • Guardiola makes history as Manchester City lift FA Cup • “Nigerians Now Teat Insecurity, Killings As Normal” – Jonathan • Students’ Abduction: We’re working with security agencies, says Makinde • Police arrest 10 over violence at Lagos APC primaries • Lagos Sanctions 15 Online Money Lending Firms Over Operational Violations • 2027: Don’t Stake Your Children’s School Fees on Primaries, Uzodimma Tells Imo APC Aspirants • Nigerian Navy Uncovers, Dismantles Illegal Refined Petroleum Products Depot in Rivers • Ex-Kwara Gov’s Aide, Ajakaye, Wins APC Federal Constituency Ticket
Tanzania, Urusi zakubaliana kushirikiana maeneo 12, mikataba miwili yasainiwa
Back to Home

Tanzania, Urusi zakubaliana kushirikiana maeneo 12, mikataba miwili yasainiwa

Mwananchi about 2 hours 5 mins read
Arusha. Tanzania na Urusi zimekubaliana kuimarisha ushirikiano katika maeneo 12 muhimu ya maendeleo, huku mikataba miwili ya ushirikiano ikisainiwa tayari na mingine zaidi ikitarajiwa kusainiwa jijini Moscow wakati wa ziara rasmi ya Rais Samia Suluhu Hassan Juni mwaka huu. Makubaliano hayo yamefikiwa katika Mkutano wa Tatu wa Pamoja wa Ushirikiano wa Biashara na Uchumi kati ya Tanzania na Urusi uliofanyika Arusha leo, Jumamosi, Mei 16, 2026. Akizungumza baada ya kusainiwa kwa mikataba hiyo miwili, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Profesa Kitila Mkumbo, amesema timu za wataalamu kutoka nchi hizo mbili zimejadili kwa kina maeneo ya ushirikiano kwa siku mbili kabla ya kufikia makubaliano hayo. “Siku mbili hizi tumejadiliana na hatimaye kukubaliana kushirikiana katika maeneo 12 ambayo tumetoka hapa kuweka sahihi. Timu zetu za wataalamu kwa muda wa siku mbili zimejadiliana kwa kina na kuandaa mambo ambayo tunakwenda kushirikiana nayo,” amesema Profesa Mkumbo. Amesema nchi hizo zimekubaliana kufanyia kazi mikataba isiyopungua 22, huku miwili ikiwa tayari imesainiwa. “Tumekubaliana kufanyia kazi mikataba isiyopungua 22, na tayari mikataba miwili imesainiwa hapa, ya ushirikiano katika maeneo ya lugha, kwa maana lugha ya Kiswahili kufundishwa katika vyuo vikuu na taasisi za elimu nchini Urusi, na lugha ya Kirusi kufundishwa katika taasisi za elimu hapa Tanzania,” amesema. Profesa Mkumbo amesema eneo hilo la lugha ni sehemu ya ushirikiano wa kiutamaduni kati ya mataifa hayo mawili. Ametaja mkataba mwingine uliosainiwa ni kati ya Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) pamoja na taasisi mbili kutoka Urusi katika sekta ya afya na uzalishaji wa dawa. “Tumesaini pia mkataba wa Chuo Kikuu cha Afya cha Muhimbili na taasisi mbili kutoka Urusi katika kushirikiana katika eneo la afya, lakini pia kuzalisha dawa,” amesema. Ameongeza kuwa mikataba mingine itasainiwa jijini Moscow wakati wa ziara rasmi ya Rais Samia Suluhu Hassan nchini Urusi kuanzia Juni 3 mwaka huu. Profesa Mkumbo amesema Tanzania na Urusi zimekuwa na historia ndefu ya ushirikiano wa kisiasa na kidiplomasia kwa muda mrefu. Hata hivyo, amesema msukumo mkubwa wa Serikali kwa sasa ni kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi, hususan biashara na uwekezaji. Kwa mujibu wa Profesa Mkumbo, maeneo ambayo nchi hizo zitashirikiana ni sekta ya kilimo, nishati, elimu, sayansi na teknolojia, usafiri na usafirishaji, pamoja na sekta ya utalii. Profesa Mkumbo amesema sekta ya kilimo ndiyo iliyopewa kipaumbele katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, huku Tanzania ikitaka kuongeza uzalishaji na thamani ya mazao yake, ambapo msisitizo ni kuhakikisha mazao yanayosafirishwa nje ya nchi yamechakatwa. “Tunaendelea kuweka nguvu nyingi katika kuongeza tija katika uzalishaji wa sekta ya kilimo, na hapa tunakazania matumizi ya mbolea. Wenzetu Urusi ni wazuri katika eneo hilo la mbolea,” amesema. Katika sekta ya nishati, amesema kampuni za Urusi zinaonesha nia kubwa ya kuwekeza katika utafutaji, uchimbaji, uchakataji na biashara ya gesi asilia, na kuwa nchi hizo zitashirikiana katika uzalishaji wa umeme wa nyuklia. Kuhusu sekta ya elimu, waziri huyo amesema Tanzania na Urusi zina historia ndefu ya ushirikiano katika elimu, huku zaidi ya Watanzania 20,000 wakipata ufadhili wa masomo nchini humo. “Kwa miaka mingi Tanzania na Urusi tumekuwa tukishirikiana katika eneo hili. Watanzania wengi wataalamu katika eneo la afya, elimu na kilimo wameweza kupata mafunzo Urusi,” amesema. Kuhusu usafiri na usafirishaji, amesema wenzao wameonyesha nia ya kuwekeza katika miundombinu ya kupanua bandari na bandari mpya, na kwamba TPA inaendelea kushirikiana na kampuni za Urusi, na mazungumzo yanaendelea vizuri. Kuhusu utalii, Profesa Mkumbo amefafanua kuwa Urusi ni moja ya vyanzo vikubwa vya watalii wanaotembelea Tanzania, ambapo zaidi ya watalii 17,000 kutoka nchini humo walitembelea Tanzania mwaka jana. “Tupo katika hatua kubwa za kuona ATCL zinafanya safari za moja kwa moja Dar es Salaam, Zanzibar hadi Moscow, na tunaamini itaongeza zaidi watalii,” amesema. Amesema mazungumzo kuhusu safari hizo yamefikia hatua za mwisho na zinatarajiwa kuanza kabla ya mwisho wa mwaka huu. Kwa upande wake, Waziri wa Maendeleo ya Uchumi wa Shirikisho la Urusi, Maksim Reshetnikov, amesema kufanyika kwa kikao hicho ni jambo muhimu kwa ajili ya kutoa msukumo mpya wa utekelezaji wa miradi na kuimarisha zaidi ushirikiano wa biashara na uchumi kati ya nchi hizo. Amesema biashara kati ya nchi hizo kwa mwaka 2025 imefikia kiwango cha juu zaidi katika historia, ambapo kiwango cha biashara kimeongezeka kwa karibu asilimia 20. “Urusi inasafirisha kwenda Tanzania ngano, mafuta ya mboga na mbolea. Nasi tunaagiza na kuongeza uagizaji wa tumbaku ghafi, kahawa, chai, matunda na bidhaa nyingine za chakula kutoka Tanzania,” amesema. Waziri huyo amesema mbali na kuongeza uagizaji wa bidhaa kutoka Tanzania kama kahawa, chai, tumbaku ghafi, korosho, matunda na mboga, wako tayari kuingia katika uzalishaji wa pamoja, kilimo cha pamoja, uchakataji na ufungashaji wa bidhaa hizo. “Urusi pia iko tayari kusambaza Tanzania mbolea, teknolojia za kuongeza rutuba ya udongo, dawa za mifugo, pamoja na kushirikiana katika uzalishaji wa mbegu bora na mifugo bora. Hatua hizi zote kwa pamoja zinalenga kuongeza tija ya kilimo nchini Tanzania na kuongeza uwezo wa kuuza bidhaa nje ya nchi,” amesema. “Eneo jingine muhimu la ushirikiano wetu ni nishati. Ukuaji wa uchumi wa Tanzania utahitaji kuongeza uzalishaji wa umeme pamoja na matumizi makubwa ya nishati. Kwa hiyo tuna nia kubwa ya kutekeleza miradi ya pamoja ya gesi asilia, kwa kuwa Tanzania ina akiba kubwa ya gesi,” amesema. Amesema katika eneo hilo, kampuni za Urusi zinaweza kuwa muhimu kama watoa teknolojia, washirika wa uwekezaji pamoja na kampuni za uhandisi, kwa sababu yana uzoefu, vifaa na teknolojia za uchimbaji, usafirishaji na uchakataji wa gesi, pamoja na ujenzi wa miundombinu ya matumizi ya gesi na usambazaji wa bidhaa za mafuta. “Mradi wetu mkubwa zaidi katika sekta ya nishati ni mradi wa Mkuju River (Mantra) unaohusisha uchimbaji na uchakataji wa uranium. Kwa sasa kazi za ujenzi wa miundombinu mikubwa ya uzalishaji zinaendelea. “Mradi huu wa Mkuju River ni mradi mkubwa wa uchimbaji wa uranium kusini mwa Tanzania, na kwa sasa tunaendelea na hatua za ujenzi wa kiwanda kikubwa kwa ajili ya uzalishaji wa uranium,” amesema. Amesema maendeleo ya ushirikiano wa biashara na uchumi hayawezi kufanikiwa bila kuboresha usafirishaji na miundombinu ya usafiri, ndiyo maana wanatoa umuhimu mkubwa kwa miradi ya pamoja ya maendeleo ya bandari.

This article was sourced from an external publication.

Share this article

Comments (0)

Want to join the discussion?

Sign in to post comments and engage with the community.

Be the first to comment!

Traditional Affairs

View All

Somalia

View All
AD
OneClick Africa Logo

Africa's premier digital hub for impactful news, entertainment, and business insights.

© 2026 OneClick Africa. All rights reserved.