TRENDING
High-flying Hull maintain unbeaten start by holding off Aston Villa in stalemate • Sifuna condemns abduction of Standard Group Associate Editor • Troops discover three decomposing bodies of terrorists in Borno • Qinwen, Potapova spring pair of US Open upsets • Ex-IGP Adamu Wins Nasarawa SDP Gov Ticket, Pledges To Tackle “Misgovernance’ • Athletic Club Thrash Atletico Madrid 3-0 In Stunning  La Liga Rout • Wike To Amaechi: You Have Lost Your Credibility In Politics • 2027: Grassroots Performance, Not Structure, Will Decide Bayelsa West – Olomu • Diphtheria: 68% Of Confirmed Cases Involve Unvaccinated People – NCDC • CAF Confederation Cup: Shooting Stars Secure Narrow First-Leg Win Over CS Sfaxien • Three die, 20 injured in Osun road crash • Makinde says 2027 ambition not limited to region • Lobbying firm replies Keyamo, alleges Tinubu govt pressure over Trump appointment • Ruparelia Group Leads Corporate Backing for India Day 2026 • UPDF Crowned Overall Champions Of 18th Inter-Forces Games In Gulu • FR LAZAR ARASU: Why National Progress is Failing the Rural Woman • Iwobi makes Premier League appearance history • Tinubu’s economic reforms are yielding results — Tope Fasua • Taraba youths capture two suspects over alleged planned attack • Simeone’s Atletico Madrid Crushed 3-0 At Athletic Bilbao • High-flying Hull maintain unbeaten start by holding off Aston Villa in stalemate • Sifuna condemns abduction of Standard Group Associate Editor • Troops discover three decomposing bodies of terrorists in Borno • Qinwen, Potapova spring pair of US Open upsets • Ex-IGP Adamu Wins Nasarawa SDP Gov Ticket, Pledges To Tackle “Misgovernance’ • Athletic Club Thrash Atletico Madrid 3-0 In Stunning  La Liga Rout • Wike To Amaechi: You Have Lost Your Credibility In Politics • 2027: Grassroots Performance, Not Structure, Will Decide Bayelsa West – Olomu • Diphtheria: 68% Of Confirmed Cases Involve Unvaccinated People – NCDC • CAF Confederation Cup: Shooting Stars Secure Narrow First-Leg Win Over CS Sfaxien • Three die, 20 injured in Osun road crash • Makinde says 2027 ambition not limited to region • Lobbying firm replies Keyamo, alleges Tinubu govt pressure over Trump appointment • Ruparelia Group Leads Corporate Backing for India Day 2026 • UPDF Crowned Overall Champions Of 18th Inter-Forces Games In Gulu • FR LAZAR ARASU: Why National Progress is Failing the Rural Woman • Iwobi makes Premier League appearance history • Tinubu’s economic reforms are yielding results — Tope Fasua • Taraba youths capture two suspects over alleged planned attack • Simeone’s Atletico Madrid Crushed 3-0 At Athletic Bilbao
Tanzania yapiga hatua mapambano utakatishaji fedha
Back to Home

Tanzania yapiga hatua mapambano utakatishaji fedha

Mwananchi about 2 hours 3 mins read
Dar es Salaam. Tanzania imepiga hatua katika kuimarisha mifumo ya kukabiliana na utakatishaji fedha haramu, ufadhili wa ugaidi na ufadhili wa silaha za maangamizi. Mafanikio haya yanashuhudiwa wakati ambao serikali imeweka bayana kuwa bado inaendelea kushughulikia maeneo 15 yaliyoainishwa katika tathmini ya kimataifa ikiwemo ikiwemo marekebisho ya sheria 12 zilizobainishwa kuwa zinahitaji maboresho kwa upande wa Tanzania Bara na Zanzibar. Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Mussa Omar ameyasema hayo jana jijini Kigali, Rwanda, wakati wa Mkutano wa 26 wa Baraza la Mawaziri la Umoja wa Nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika wa Kupambana na Utakasishaji Fedha Haramu, Ufadhili wa Ugaidi na Silaha za Maangamizi (ESAAMLG). Amesema Tanzania imefanikiwa katika tathmini ya pamoja iliyofanywa na ESAAMLG kupitia Kamati ya Wataalamu huku Serikali ikiendelea kutekeleza maboresho yaliyobainishwa ili kuimarisha sekta ya fedha na kusaidia maendeleo ya kiuchumi na kijamii. “Tuna sheria na kamati ya kitaifa ya kupambana na masuala haya. Mafanikio ni makubwa lakini bado kuna maeneo 15 tunayafanyia kazi ikiwemo marekebisho ya sheria 12 zilizobainishwa kuwa zinahitaji maboresho kwa upande wa Tanzania Bara na Zanzibar,” amesema. Kati ya maeneo hayo, Tanzania Bara tayari imepitisha sheria nne kupitia Bunge katika kikao kinachoendelea huku Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ikitarajiwa kuwasilisha miswada ya marekebisho ya sheria nyingine tatu. Amesema hatua hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa mapendekezo yaliyotolewa baada ya tathmini ya mifumo ya Tanzania ya kuzuia na kukabiliana na uhalifu wa kifedha. Amesema mafanikio hayo yametokana na ushirikiano wa taasisi mbalimbali za Serikali, zikiwemo Wizara ya Fedha, wasimamizi wa sekta ya benki, Wizara ya Katiba na Sheria, Wizara ya Mambo ya Ndani na taasisi nyingine zinazounda Kamati ya Kitaifa ya kupambana na utakasishaji fedha haramu na vitendo vinavyohusiana. “Kuimarishwa kwa mifumo hiyo ni muhimu katika kulinda sekta ya fedha dhidi ya fedha zinazotokana na uhalifu na kuhakikisha Tanzania inaendelea kuwa na mfumo unaokidhi viwango vya kimataifa,’ amesema. Mkutano huo wa Kigali umewakutanisha mawaziri, makatibu wakuu na maafisa waandamizi kutoka nchi wanachama wa ukanda wa Mashariki na Kusini mwa Afrika kwa ajili ya kujadili namna ya kuimarisha ushirikiano katika mapambano dhidi ya utakasishaji fedha haramu, ufadhili wa ugaidi na ufadhili wa silaha za maangamizi. Kutoka Tanzania, viongozi walioshiriki ni Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Juma Homera, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dk Seif Abdallah Shekalaghe, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango-Zanzibar, Aboud Hassan Mwinyi na Kamishna wa Kitengo cha Ujasusi wa Fedha (FIU), Majaba Magana. Wengine ni Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Wataalamu ya Kuzuia Utakatishaji Fedha Haramu, Sauda Msemo pamoja na wakuu wa taasisi, wataalamu wa sekta ya fedha, wasimamizi wa taasisi za kifedha na wadau wa maendeleo. Mkutano huo pia unalenga kuimarisha ushirikiano wa nchi wanachama katika kubadilishana taarifa na uzoefu wa kukabiliana na uhalifu wa kifedha unaoweza kuhatarisha uchumi, usalama na mifumo ya fedha ya nchi.

This article was sourced from an external publication.

Share this article
OneClick Africa Logo

Africa's premier digital hub for impactful news, entertainment, and business insights.

© 2026 OneClick Africa. All rights reserved.