TRENDING
Police rescue 23-year-old after jumping into Lagos lagoon • ‘Poverty not Nigeria’s destiny’ – SDP chieftain, Adebayo blasts Tinubu govt • Elon Musk Bets On SpaceX IPO • Senate queries SEDC, accuses commission of spending N153m on Abuja office rent • Top 10 most affordable HMOs for individuals in Nigeria – June 2026 • Commercial driver dies in autocrash on Lagos-Apapa Expressway • Kebbi: Police confirm death of abducted Islamic cleric in bandits’ captivity • NDC: Why Kwankwaso should take charge of structures in Kano – Sambo • China Inflation Stabilises In May As Energy Costs Ease • The real cost of building on borrowed land • Improving your competitive advantage as a service provider (Part VI) • Anambra awards over N1bn contracts for flood control, others • Education as an ESG investment • World Cup 2026: ‘I can’t influence it’ – Ndidi names two players Martinez should’ve named in Portugal squad • 2027: Peter Obi needs to expand electoral map across Northern Nigeria – Sam Amadi • Nigeria Claims Three Gold Medals At African Taekwondo Championships In Mali • How IMF pressure shaped Ruto's tax hikes • Accord Party supporters rally behind Olawepo-Hashim in Kaduna • War: Iran fires missiles, drones at United States • Friendly: Portugal coach, Martinez names player that’ll play full 90 minutes against Nigeria • Police rescue 23-year-old after jumping into Lagos lagoon • ‘Poverty not Nigeria’s destiny’ – SDP chieftain, Adebayo blasts Tinubu govt • Elon Musk Bets On SpaceX IPO • Senate queries SEDC, accuses commission of spending N153m on Abuja office rent • Top 10 most affordable HMOs for individuals in Nigeria – June 2026 • Commercial driver dies in autocrash on Lagos-Apapa Expressway • Kebbi: Police confirm death of abducted Islamic cleric in bandits’ captivity • NDC: Why Kwankwaso should take charge of structures in Kano – Sambo • China Inflation Stabilises In May As Energy Costs Ease • The real cost of building on borrowed land • Improving your competitive advantage as a service provider (Part VI) • Anambra awards over N1bn contracts for flood control, others • Education as an ESG investment • World Cup 2026: ‘I can’t influence it’ – Ndidi names two players Martinez should’ve named in Portugal squad • 2027: Peter Obi needs to expand electoral map across Northern Nigeria – Sam Amadi • Nigeria Claims Three Gold Medals At African Taekwondo Championships In Mali • How IMF pressure shaped Ruto's tax hikes • Accord Party supporters rally behind Olawepo-Hashim in Kaduna • War: Iran fires missiles, drones at United States • Friendly: Portugal coach, Martinez names player that’ll play full 90 minutes against Nigeria
Ufahamu ugonjwa wa akili unaoweza kusababishwa na bangi
Back to Home

Ufahamu ugonjwa wa akili unaoweza kusababishwa na bangi

Mwananchi about 3 hours 4 mins read
Dar es Salaam. Schizophrenia ni ugonjwa sugu wa muda mrefu unaoathiri afya ya akili ya mtu ambao unaathiri uwezo wa kufikiri, kujifikia na kutenda kadiri ya matarajio ya watu wanaokuzunguka. Ugonjwa huo unaathiri utambuzi wa mtu kiasi cha kushindwa kutofautisha uhalisia, kupoteza uwezo wa uhusiano wake na wanajamii wengine ambapo mtu mwenye hali hii akili huwa haitulii kwani anaweza kuwa anasikia kelele yeye peke yake, akatoa kauli kusema vitu visivyoeleweka au kuchelewa kuelewa vitu. Anayeugua tatizo hili hukosa muunganiko wa matukio na hali halisi ya maisha yake kwani kuna wakati huwa katika hali ya kawaida na wakati mwingine hufanya vitu vinavyoshangaza wengi. Kwa mujibu wa Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO), Schizophrenia inaathiri takribani watu milioni 23 duniani, sawa na mtu mmoja kati ya 345. Ugonjwa huo hauna sababu kuu inayojulikana lakini wataalamu wanauweka kuwa wa kurithi kutoka kwenye vizazi kwa sababu ya kutembea kwenye damu, pia umbile la ubongo wa mtu alivyozaliwa kuwa chini ya kilo moja au kuzidi. Sababu nyingine ni matumizi ya dawa za kulevya kama bangi, sigara, pombe na mazingira aloyokulia mtu ikiwemo msongo wa mawazo, kupambana na majanga mbalimbali, kama anavyosema Daktari bingwa mbobezi wa saikolojia na afya ya akili kutoka Hospitali ya Taifa ya Afya ya Akili Mirembe, Swai Japhet wakati akizungumza na Mwananch. “Kimsingi pombe na sigara inamuathiri zaidi mtu mwenye Schizophrenia kwenye damu lakini haijawahi kuonekana kwahiyo kama atatumia vitu hivyo vitaenda kuamsha ugonjwa huo. Lakini haina maana vitu hivyo vinasababisha moja kwa moja,” amesema. Bangi Akifafanua zaidi kuhusu bangi, Bingwa huyo amesema yenyewe haihitaji uwe umerithi schizophrenia kwenye damu bali yenyewe inauwezo wa kusababisha moja kwa moja. “Bangi ukivuta baada ya muda unapata schizophrenia na inategemea kichwa cha mtu mwingine anaweza kuvuta kwa miezi sita akapata au mwingine akakaa hata miaka 20 akaugua,” amesema. Dalili Dk Japhet anasema mgonjwa anaweza akawa anaona au kusikia vitu ambavyo wengine hawaoni wala kusikia. “Anaweza kusikia sauti za watu wengi wanamjadili, sauti inayomuelekeza kitu cha kufanya au sauti kutoka kwenye mwili wake yeye mwenyewe,” amesema. Pia, kuna hisia danganyifu ikiwemo kusikia harufu ambayo wengine hawaisikii, pia kuonja ladha ya kitu ambacho ajala na kugusa au kutoa kitu kwenye ngozi yake. Dalili nyingine anakuwa na imani ngumu kumbadilisha ikiwemo kusema yeye ni mtoto wa Rais Trump, au yeye ni Rais, au ametengeneza dawa ya ugonjwa fulani wakati hata kwa muonekano wake inaonesha hajasoma. “Anakuwa anaamini kwelikweli, dalili nyingine ni kujitenga, kupoteza uwezo wa kujituma pia kuna dalili hasi ambapo uso wake hauonekani kama umefurahi au umekasirika”. Akiongeza zaidi amesema zipo dalili za kiakili kama kupoteza uwezo wake wa kufanya maamuzi na kuchakata taarifa na kuzingatia pia kupoteza kumbukumbu. Tiba Ugonjwa huo unatibiwa na dawa za magonjwa ya akili kwenye vitengo maalumu vya kuhudumia watu wenye magonjwa ya akili. Pia, Jamii inapaswa ijue kuhusu hii ili wapunguze unyanyapaa, wagonjwa pia wanapaswa kutibiwa kupitia tiba ya saikolojia kupitia maongezi pale akili zinapoanza kurudi. Dk Japhet amesema kuhusu imani za kijamii ni tatizo linaloathiri matibabu ya ugonjwa huo kutokana na kwenda kwa waganga wa kienjyeji na wahubiri hali inayosababisha magonjwa kucheleweshwa kwenda hospitali kwa muda mrefu. “Mgojwa wa schizophrenia anafanya vitu ambavyo havijazoeleka kwenye jamii jambo ambalo watu wahisi amerogwa, mapepo au laana ndio maana jamii inawapeleka huko wagonjwa hawa. Kwa mujibu wa WHO, kwa sasa, watu wengi wenye schizophrenia duniani hawapati huduma za afya ya akili. Takribani asilimia 50 ya wagonjwa waliolazwa katika hospitali za afya ya akili wana schizophrenia. Ni asilimia 29 pekee ya watu wenye psychosis hupata huduma maalumu za afya ya akili. WHO inaeleza kuwa hospitali nyingi za afya ya akili hazijawa na ufanisi katika kutoa huduma bora na mara nyingi zimekuwa zikikiuka haki za msingi za wagonjwa. Shirika hilo linahimiza huduma zihamishiwe zaidi kwenye jamii kupitia vituo vya afya, hospitali za kawaida, huduma za nyumbani na vituo vya ushauri wa afya ya akili.

This article was sourced from an external publication.

Share this article

Comments (0)

Want to join the discussion?

Sign in to post comments and engage with the community.

Be the first to comment!

DR Congo

View All

Senegal

View All
AD
OneClick Africa Logo

Africa's premier digital hub for impactful news, entertainment, and business insights.

© 2026 OneClick Africa. All rights reserved.