TRENDING
Police arrest suspected bandit informants, recover 97 livestock in Sokoto • Plateau: Thugs disrupt APC Primary in Jos South LGA • Big Brother Naija is back; registration portal opens • 850-bed UCTH overstretched, serves over 5m patients -CMD • UCH resident doctors declare warning strike over assault • Coventry City Sign Onyeka On Permanent Transfer • أنظمة الطاقة الشمسية والإنترنت الفضائي، يغيران قواعد سوق الاتصالات في السودان • PDP clears Adebutu for Ogun guber primary ahead of 2027 poll • Cubana Chief Priest loses bid for APC reps ticket in Imo • AFRICOM unveils footage of deadly Joint strike that killed top ISIS Commander in Nigeria • 2027: APC releases list of disqualified Reps aspirants • Iran confirms squad heading to Turkey for World Cup preparation • Ghana Hajj Medical Team secures historic full licence to operate clinics in Makkah • Hajj 2026: Final Ghana airlift extended to Tuesday - Amin Lamptey • We must not let the memory of May 15, 1979 die - United Cadres Front • Water crisis looms in parts of Volta as GWL shuts down Kpeve treatment plant • Police Mourn 17 Officers Killed In Yobe Terrorist Attack • ‘Not same Abu-Bilal Al-Minuki killed in 2024’ – DHQ clarifies identity of dead ISWAP commander • How APC Reps candidates emerged during primaries in Delta • Netanyahu calls for gradual end to US military aid to Israel • Police arrest suspected bandit informants, recover 97 livestock in Sokoto • Plateau: Thugs disrupt APC Primary in Jos South LGA • Big Brother Naija is back; registration portal opens • 850-bed UCTH overstretched, serves over 5m patients -CMD • UCH resident doctors declare warning strike over assault • Coventry City Sign Onyeka On Permanent Transfer • أنظمة الطاقة الشمسية والإنترنت الفضائي، يغيران قواعد سوق الاتصالات في السودان • PDP clears Adebutu for Ogun guber primary ahead of 2027 poll • Cubana Chief Priest loses bid for APC reps ticket in Imo • AFRICOM unveils footage of deadly Joint strike that killed top ISIS Commander in Nigeria • 2027: APC releases list of disqualified Reps aspirants • Iran confirms squad heading to Turkey for World Cup preparation • Ghana Hajj Medical Team secures historic full licence to operate clinics in Makkah • Hajj 2026: Final Ghana airlift extended to Tuesday - Amin Lamptey • We must not let the memory of May 15, 1979 die - United Cadres Front • Water crisis looms in parts of Volta as GWL shuts down Kpeve treatment plant • Police Mourn 17 Officers Killed In Yobe Terrorist Attack • ‘Not same Abu-Bilal Al-Minuki killed in 2024’ – DHQ clarifies identity of dead ISWAP commander • How APC Reps candidates emerged during primaries in Delta • Netanyahu calls for gradual end to US military aid to Israel
Ujumbe wa Trump watupa zawadi ulizopewa China, kabla ya kupanda ndege
Back to Home

Ujumbe wa Trump watupa zawadi ulizopewa China, kabla ya kupanda ndege

Mwananchi about 4 hours 4 mins read
Washington. Rais Donald Trump na ujumbe wa maofisa wa Marekani wameondoka Beijing, China, baada ya kukamilisha ziara ya siku mbili iliyohusisha mazungumzo ya ngazi ya juu kati yake na Rais Xi Jinping. Hata hivyo, hatua kali za kiusalama zilizochukuliwa kabla ya safari ya kurejea Marekani zimeibua mjadala mkubwa kuhusu kiwango cha tahadhari ya Washington dhidi ya Beijing. Kwa mujibu wa ripoti kutoka kwa waandishi waliokuwa katika msafara wa Ikulu ya White House, wafanyakazi wa Marekani walikusanya na kutupa vitu vyote vilivyotolewa na wenyeji wao wa China kabla ya mtu yeyote kuruhusiwa kupanda ndege ya Rais, Air Force One, katika Uwanja wa Ndege wa Beijing Capital. Miongoni mwa vitu vilivyotupwa ni pamoja na simu maalumu za muda (burner phones), vitambulisho vya safari, pamoja na pini za ukumbusho zilizokuwa zimevaliwa na baadhi ya wajumbe wa Marekani wakati wa ziara hiyo. Mwandishi wa White House wa gazeti la New York Post, Emily Goodin, aliandika katika mtandao wa X: “Hakuna kitu chochote kutoka China kilichoruhusiwa kuingia ndani ya ndege.” Hatua hiyo inaaminika kuchukuliwa kwa misingi ya tahadhari za kiusalama, huku China ikiendelea kutazamwa na Marekani kama mmoja wa wapinzani wake wakubwa katika masuala ya intelijensia na ujasusi wa kimtandao. Marekani na washirika wake wamekuwa wakiishutumu Beijing kwa kuhusika katika mashambulizi ya kimtandao na shughuli za upelelezi dhidi ya mataifa ya Magharibi. Wachambuzi wa usalama wanaeleza kuwa ni kawaida kwa mataifa makubwa kuwa na hofu ya vifaa au zawadi zinazoweza kuwa zimewekewa vifaa vya udukuzi au ufuatiliaji wa siri. Simu za muda zinazotumiwa katika safari nyeti za kidiplomasia mara nyingi hutupwa baada ya matumizi, ili kuondoa uwezekano wa kudukuliwa. Licha ya tahadhari hizo, kuondoka kwa Trump kulionekana kuwa na ishara za urafiki wa kidiplomasia. Waziri wa Mambo ya Nje wa China, Wang Yi, alikuwa uwanjani kumuaga Rais huyo wa Marekani huku wanafunzi wa shule wakiwa wamevalia rangi zinazofanana na ndege ya Air Force One, wakipeperusha bendera za Marekani na China na kuimba salamu za kuagana. Trump alionekana mwenye furaha alipofika kwenye ngazi za ndege hiyo, akipunga mkono na kuinua ngumi yake hewani, kabla ya kuingia ndani ya ndege bila kutoa tamko lolote zaidi kwa waandishi wa habari. Ziara hiyo ilikuwa ya kwanza kwa Rais wa Marekani aliye madarakani kutembelea China katika kipindi cha miaka tisa, na ya kwanza kwa Trump tangu ziara yake ya mwaka 2017. Trump na Xi walifanya mazungumzo yaliyodumu takribani saa mbili katika Ukumbi Mkuu wa Watu (Great Hall of the People), kabla ya kushiriki shughuli mbalimbali za kidiplomasia ikiwamo matembezi katika maeneo ya kihistoria ya Beijing. Rais Xi Jinping aliitaja ziara hiyo kuwa ya “kihistoria na yenye alama muhimu,” akisema pande zote mbili zimekubaliana kujenga uhusiano wa “utulivu wa kimkakati” kati ya China na Marekani. Kwa upande wake, Trump alisema ziara hiyo imezaa mafanikio kadhaa na kusisitiza kuwa ana heshima kubwa kwa Xi Jinping. Viongozi hao pia walijadili masuala ya kimataifa, ikiwamo mvutano kuhusu Iran na hali ya usalama katika eneo la Taiwan. Hata hivyo, pamoja na ishara hizo za urafiki, duru za kimataifa zinaeleza kuwa mkutano huo haukuzaa mafanikio makubwa katika masuala nyeti ya biashara, udhibiti wa bidhaa adimu za madini kutoka China, wala hatua madhubuti kuhusu mgogoro wa Iran. Ripoti zinaeleza kuwa Xi Jinping alimwonya Trump kwa faragha kuhusu hatari ya mgogoro wowote unaohusu Taiwan kugeuka vita, huku Trump akiepuka kutoa msimamo mkali hadharani kuhusu suala hilo wakati wote wa ziara yake. Aidha, hakukuwa na makubaliano rasmi kuhusu biashara ya mazao ya kilimo, nyama ya ng’ombe wala sekta ya anga, licha ya matarajio makubwa yaliyokuwepo kabla ya mkutano huo. Wakati Trump akitafuta ushindi wa haraka wa kisiasa kuelekea uchaguzi wa katikati ya muhula nchini Marekani, Xi Jinping alionekana kuelekeza nguvu katika kujenga taswira ya muda mrefu ya uhusiano mpya kati ya mataifa hayo mawili yenye nguvu kubwa duniani.

This article was sourced from an external publication.

Share this article

Comments (0)

Want to join the discussion?

Sign in to post comments and engage with the community.

Be the first to comment!

Traditional Affairs

View All

Somalia

View All
AD
OneClick Africa Logo

Africa's premier digital hub for impactful news, entertainment, and business insights.

© 2026 OneClick Africa. All rights reserved.