TRENDING
Lagos seals six iron, steel companies in Ikorodu over environmental violations • ntel seeks fresh capital to fuel digital infrastructure expansion after AMCON recovery • Regulatory dispute renews fear over Nigeria’s telecom credit services • Reps give IGP 24 hours to present embattled FCIPC DG, Adeyemi • MTN earns 82% outside South Africa as CEO warns xenophobia could undermine Africa’s $3.4trn single market vision • Police dismantle Asaba phone-stealing syndicate, nab four members • Edo to demolish buildings on waterways, flood channels • Glasgow 2026: Lawal powers team Nigeria to sixth gold with games record lift • Violence mars Delta APC leadership meeting, scores injured • Two things that caught my attention from Peter Obi’s interview – Bayo Onanuga • 12-yr-old Nigerian wins bronze at World Performing Arts Championships • Transfer: He’s flexible, great signing – Xabi Alonso on Chelsea’s new signing • FLASHBACK: ‘I leave my clothes and shoes with women who have my children’ — Kwam 1 • NSCDC Arrests Driver In Anambra Over Alleged Attempt To Run Over Officers • UNILAG withdraws ‘Do not shake hands’ anti-rape advisory after backlash • NANS plans protest over ex-FUOYE SUG president’s remand • Katsina security outfit kills over 40 bandits, repels attack • Mind the ever-growing gap: the Premier League keeps spending big • Three promising business opportunities in Somalia • He gave you golden opportunity – Presidency reacts to Peter Obi’s interview • Lagos seals six iron, steel companies in Ikorodu over environmental violations • ntel seeks fresh capital to fuel digital infrastructure expansion after AMCON recovery • Regulatory dispute renews fear over Nigeria’s telecom credit services • Reps give IGP 24 hours to present embattled FCIPC DG, Adeyemi • MTN earns 82% outside South Africa as CEO warns xenophobia could undermine Africa’s $3.4trn single market vision • Police dismantle Asaba phone-stealing syndicate, nab four members • Edo to demolish buildings on waterways, flood channels • Glasgow 2026: Lawal powers team Nigeria to sixth gold with games record lift • Violence mars Delta APC leadership meeting, scores injured • Two things that caught my attention from Peter Obi’s interview – Bayo Onanuga • 12-yr-old Nigerian wins bronze at World Performing Arts Championships • Transfer: He’s flexible, great signing – Xabi Alonso on Chelsea’s new signing • FLASHBACK: ‘I leave my clothes and shoes with women who have my children’ — Kwam 1 • NSCDC Arrests Driver In Anambra Over Alleged Attempt To Run Over Officers • UNILAG withdraws ‘Do not shake hands’ anti-rape advisory after backlash • NANS plans protest over ex-FUOYE SUG president’s remand • Katsina security outfit kills over 40 bandits, repels attack • Mind the ever-growing gap: the Premier League keeps spending big • Three promising business opportunities in Somalia • He gave you golden opportunity – Presidency reacts to Peter Obi’s interview
Ushahidi wa mtoto aliyekuwa akilawitiwa makaburini wamfunga maisha bodaboda
Back to Home

Ushahidi wa mtoto aliyekuwa akilawitiwa makaburini wamfunga maisha bodaboda

Mwananchi about 4 hours 4 mins read
Arusha. Ushahidi wa mtoto wa miaka saba, aliyesimulia namna dereva wa bodaboda, Laurent Kapinga, aliyekuwa akimpeleka shuleni, alivyokuwa akimpitisha makaburini na kumlawiti, umeifanya Mahakama Kuu kubatilisha uamuzi wa kumwachia huru na badala yake kumhukumu kifungo cha maisha. Mbali na ushahidi wa mtoto huyo, ushahidi mwingine ni wa kitabibu wa daktari aliyemchunguza na kubaini kulikuwa na michubuko sehemu yake ya haja kubwa na kuwa uliunga mkono ushahidi wa mwathirika wa tukio hilo. Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Songea, imesema Mahakama ya Wilaya ya Mbinga ilikosea kuupuuza ushahidi huo kwa kuzingatia kasoro ndogo katika fomu ya polisi namba tatu (PF3), ilhali ushahidi wa mtoto ulikuwa wa kuaminika, uliungwa mkono na ushahidi wa kitabibu na ulitosha kuthibitisha kosa la ulawiti bila kuacha shaka yoyote. Hukumu hiyo imetolewa Julai 21, 2026 na Jaji Emmanuel Kawishe aliyekuwa akisikiliza rufaa ya jinai namba 30655/2026 iliyokatwa na Jamhuri dhidi ya Laurent. Baada ya kupitia mwenendo, rufaa na sababu za pande zote mbili, Mahakama hiyo ilifuta uamuzi wa Mahakama ya chini na kumtia hatiani Laurent ambaye katika hukumu hiyo anajulikana kwa maarufu la Lau, akisema adhabu ya kifungo cha maisha itaanza kutekelezwa atakapokamatwa. Amesema Mahakama ya Wilaya ya Mbinga ilifanya makosa ya kisheria kwa kutupilia mbali ushahidi huo kwa kuzingatia kasoro ndogo zilizokuwa kwenye fomu ya PF3, badala ya kuutathmini ushahidi wote kwa pamoja na kuwa ushahidi wa mtoto ulikuwa wa kuaminika na ulithibitishwa na ushahidi wa kitabibu hivyo ulitosha kuthibitisha kosa. Kutokana na uamuzi huo, Mahakama Kuu ilikubali rufaa ya Jamhuri, ikafuta uamuzi wa Mahakama ya Wilaya uliomwachia huru Laurent na kumhukumu kifungo cha maisha. Msingi wa rufaa Awali dereva bodaboda huyo alishtakiwa katika Mahakama hiyo ya chini akikabiliwa na kosa la ulawiti kinyume na Kifungu cha 154(1)(a) na (2) cha Kanuni ya Adhabu, kosa lililodaiwa kutokea kwa tarehe tofauti za Novemba na Disemba 2023 katika Mtaa wa Mbambi wilayani Mbinga, Mkoa wa Ruvuma. Upande wa mashtaka ulikuwa na mashahidi watano ambapo shahidi wa tatu ambaye ni babu wa mwathirika wa tukio hilo aliyekuwa akiishi naye, aliiambia Mahakama kuwa alianza kubaini hali isiyo ya kawaida kwa mjukuu wake ikiwemo kutokwa na haja kubwa. Alidai baada ya kubaini hivyo alimjulisha baba wa mtoto huyo ambaye alimpeleka Hospitali kwa ajili ya uchunguzi ambapo iligundulika kuwa na michubuko sehemu ya nje ya njia ya haja kubwa na kuhitimisha kuwa kitu butu kilipenya. Katika ushahidi wa mtoto huyo aliiambia mahakama kuwa Kaka Lau (mjibu rufaa) aliyekuwa akimpeleka shule, alipita naye makaburini na kwenye moja ya makaburi hayo alimuamuru avue kaptula yake na kumfanyia kitendo hicho na alimfanyia hivyo mara mbili. Alidai alitishiwa kuuawa endapo angemweleza mtu yoyote kuhusu matukio hayo. Mbali na ushahidi huo, Mahakama ya Wilaya ilimwachia huru mshtakiwa ikisema ushahidi wa mtoto ulihitaji kuthibitishwa na kulikuwa na dosari katika fomu ya PF3 pamoja na ushahidi wa daktari. Jamhuri haikuridhishwa na uamuzi huo na kukata rufaa Mahakama Kuu. Rufaa Wakili wa Serikali alidai kuwa mahakama ya chini ilikosea kisheria kumwachia Lau licha ya ushahidi wa mtoto pamoja na daktari kuthibitisha kosa hilo bila kuacha shaka. Alisema mahakama ilijielekeza vibaya iliposhikilia kuwa ushahidi wa mtoto ulipaswa kuthibitishwa na ushahidi mwingine, wakati sheria na maamuzi ya Mahakama ya Rufaa yanaelekeza kuwa makosa ya kingono ushahidi wa mwathirika wa tukio unaweza kutosha kuthibitisha hatia iwapo unaaminika. Alisema kuwa mtoto alichelewa kutoa taarifa kwa sababu mshtakiwa alikuwa amemtishia kumuua, jambo ambalo halikupaswa kutafsiriwa kuwa ushahidi wake haukuwa wa kuaminika. Uamuzi Mahakama Jaji Kawishe alisema Mahakama ya Wilaya ya Mbinga ilikosea kutathmini ushahidi uliowasilishwa na upande wa mashtaka na kujikita zaidi katika kasoro ndogo zilizokuwa kwenye fomu ya PF3 badala ya kuangalia ushahidi wote kwa ujumla. Aidha alikubaliana kuwa kulikuwa na kasoro katika fomu ya PF3 kwa kuwa sehemu moja ilieleza uchunguzi wa ubakaji badala ya ulawiti na kutokana na kasoro hiyo, alisema PF3 haikuweza kutegemewa kama kielelezo na akaiondoa kwenye rekodi ya ushahidi. Hata hivyo, alisema kuondolewa kwa PF3 hakukuondoa nguvu ya ushahidi wa mtoto pamoja na ule wa daktari na kuwa maelezo ya mtoto kuhusu jinsi alivyolawitiwa yalikuwa ya kuaminika na yaliungwa mkono na ushahidi wa daktari aliyebaini michubuko kwenye njia ya haja kubwa. Jaji huyo alisisitiza kuwa katika makosa ya kingono, ushahidi wa mwathiriwa unaweza kutosha peke yake iwapo mahakama itajiridhisha kuwa ni wa kuaminika. Aidha, alisema kushindwa kwa daktari kukumbuka jina la mtoto wakati wa kutoa ushahidi hakukuweza kuharibu kesi kwa kuwa alikuwa amemuhudumia muda mrefu kabla ya kufika mahakamani. Kwa msingi huo, aliruhusu rufaa ya Jamhuri, akabatilisha uamuzi uliomwachia huru mshtakiwa, akamtia hatiani kwa kosa la ulawiti na kumhukumu kifungo cha maisha jela, adhabu itakayoanza kutekelezwa mara atakapokamatwa.

This article was sourced from an external publication.

Share this article

Comments (0)

Want to join the discussion?

Sign in to post comments and engage with the community.

Be the first to comment!

Cameroon

View All

Senegal

View All
AD

DR Congo

View All

Traditional Affairs

View All
AD
OneClick Africa Logo

Africa's premier digital hub for impactful news, entertainment, and business insights.

© 2026 OneClick Africa. All rights reserved.