TRENDING
Ebola cases in DR Congo top 5,000 – Africa CDC • Breaking: Tinubu Appoints Olumuyiwa Enitan As Head of Service, Effective August 27 • Rapper Ms Jorji accuses Poco Lee of attempted sexual assault in Dallas • Adeleke campaign spokesman vows to defeat Osun Rep in 2027 • Aliyu links Sokoto development projects to FG revenue • WHO says DRC Ebola outbreak remains far from control • KASU: Kaduna Govt urges ASUU to embrace dialogue • Wasira awataka wana-CCM kuhakiki taarifa za mitandaoni • Reporter’s Diary: Reporting COP17 from Ulaanbaatar, Mongolia • Land grabbing: Villagers urge Abia Govt to enforce court order, avert violence • Lagos goes traditional as 3m residents celebrate Ìṣẹ̀ṣe Day • Anambra @35: Govt to produce 20 documentaries on erosion • Done Deal: Nigerian Defender Joins Ugandan Club Vipers SC • Imo spends N2.19bn on security as N1.47trn budget records 14.4% performance in first half of 2026 • Soludo’s wife announces free computer training for youths in Anambra • LAWMA, police strengthen fight against illegal waste dumping • Fuel Subsidy reform averted deeper economic crisis – FG • Fubara urges parties to respect Rivers peace process, says state now at rest • LASU VC Olatunji-Bello bows out after five years • 2027: NDC unveils Ogah as Abia guber candidate, vows to replicate ‘Osun template’ • Ebola cases in DR Congo top 5,000 – Africa CDC • Breaking: Tinubu Appoints Olumuyiwa Enitan As Head of Service, Effective August 27 • Rapper Ms Jorji accuses Poco Lee of attempted sexual assault in Dallas • Adeleke campaign spokesman vows to defeat Osun Rep in 2027 • Aliyu links Sokoto development projects to FG revenue • WHO says DRC Ebola outbreak remains far from control • KASU: Kaduna Govt urges ASUU to embrace dialogue • Wasira awataka wana-CCM kuhakiki taarifa za mitandaoni • Reporter’s Diary: Reporting COP17 from Ulaanbaatar, Mongolia • Land grabbing: Villagers urge Abia Govt to enforce court order, avert violence • Lagos goes traditional as 3m residents celebrate Ìṣẹ̀ṣe Day • Anambra @35: Govt to produce 20 documentaries on erosion • Done Deal: Nigerian Defender Joins Ugandan Club Vipers SC • Imo spends N2.19bn on security as N1.47trn budget records 14.4% performance in first half of 2026 • Soludo’s wife announces free computer training for youths in Anambra • LAWMA, police strengthen fight against illegal waste dumping • Fuel Subsidy reform averted deeper economic crisis – FG • Fubara urges parties to respect Rivers peace process, says state now at rest • LASU VC Olatunji-Bello bows out after five years • 2027: NDC unveils Ogah as Abia guber candidate, vows to replicate ‘Osun template’
Aliyembaka mtoto wa mwaka mmoja akwama rufaa, ahukumiwa jela maisha
Back to Home

Aliyembaka mtoto wa mwaka mmoja akwama rufaa, ahukumiwa jela maisha

Mwananchi about 2 hours 4 mins read
Arusha. Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Tanga, imetupilia mbali rufaa ya Greyson Msemo aliyekuwa akipinga hukumu ya kifungo cha miaka 30 jela baada ya kukutwa na hatia ya kumbaka mtoto wa mwaka mmoja na miezi minne na badala yake imeongeza adhabu hiyo kuwa kifungo cha maisha. Greyson alishtakiwa mahakama ya Wilaya Pangani kwa kosa la ubakaji kinyume na kifungu cha 130(1) (2) (e) na 131 (1) cha Kanuni ya Adhabu, kosa alilodaiwa kulitenda Septemba Mosi, 2025 katika eneo la Funguni,Wilaya ya Pangani Mkoa wa Tanga. Uamuzi uliobatilisha adhabu hiyo na kumuongezea kuwa kifungo cha maisha jela umetolewa na Jaji Happiness Ndesamburo, Agosti 18,2026. Jaji Ndesamburo amesema baada ya kupitia kwa makini hoja za pande zote na kumbukumbu nzima ya kesi, ameridhika kuwa upande wa mashtaka ulithibitisha shtaka dhidi ya Greyson bila kuacha shaka yoyote. Jaji amesema ingawa mtoto aliyedaiwa kufanyiwa ukatili huo hakutoa ushahidi mahakamani kutokana na umri wake wa mwaka mmoja na miezi minne, hali hiyo haikufanya kesi ya upande wa mashtaka kuwa na dosari. Kesi ilivyokuwa Katika kuthibitisha kesi hiyo upande wa mashtaka ulikuwa na mashahidi wanne ambapo shahidi wa kwanza alikuwa bibi wa mtoto huyo na siku ya tukio akiwa anasuka mitende, alimtuma mjukuu wake mwingine kumletea Msemo maji ya kunywa. Alidai mtoto huyo aliporudi, naye alitoka nje na kumkuta Msemo akiwa amemshikilia mwathirika wa tukio hilo mapajani huku akifanya kitendo hicho cha kikatili kwa mtoto huyo. Alidai alipopiga kelele, Msemo alivuta suruali yake, ambapo alimwita mumewe na baada ya watu kukusanyika eneo hilo Msemo alikamatwa na kupelekwa Kituo cha Polisi Pangani. Shahidi wa nne ambaye ni mama wa mwathirika wa tukio hilo, alisema kuwa alimwacha mtoto wake chini ya uangalizi wa mama yake na kwenda msibani Muheza ambapo alipopata taarifa kuhusu tukio hilo na kurudi, alikuta mtoto tayari amefikishwa hospitalini kwa matibabu. Kwa upande wa utetezi, Msemo alikana kutenda kosa hilo na kudai hakuwajua watu waliohusika katika jambo hilo na kuwa ushahidi wa upande wa mashtaka haukuwa wa kweli. Rufaa Akiwa hajaridhishwa na uamuzi huo alikata rufaa akiwa na sababu tano ikiwemo hakimu alikosea kisheria kwa kumtia hatiani bila ushahidi kutoka kwa mwathirika wa tukio hilo, ushahidi wa mashtaka ulikuwa dhaifu na wenye shaka. Sababu nyingine alidai kuwa Hakimu alikosea kwa kushindwa kubaini kuwa mrufani (mshtakiwa kwa wakati huo) hakuwa mzima wa akili na kuwa kesi dhidi yake haikuthibitishwa bila kuacha shaka yoyote. Uamuzi wa Mahakama Jaji Ndesamburo amesema sheria inatambua mazingira ambayo kosa linaweza kuthibitishwa bila mwathirika kutoa ushahidi, ikiwamo pale mwathirika akiwa na umri mdogo sana. Kuhusu ushahidi wa tukio, Jaji amesema ushahidi wa bibi wa mtoto ulikuwa wa moja kwa moja na wa kuaminika, kwani alimkuta Msemo katika eneo la tukio na baadaye alipiga kelele , huku ushahidi huo ukiungwa mkono na ushahidi wa kitabibu. Jaji amesema matokeo ya uchunguzi wa kitabibu yalionyesha kuwepo kwa majeraha katika sehemu za siri za mtoto na kuwa ni sheria iliyoidhinishwa kwamba hata kupenya kidogo kunatosha kuhalalisha kosa hilo la ubakaji. Jaji pia alikataa hoja ya Msemo kwamba upande wa mashtaka ulipaswa kuwaita majirani, kiongozi wa kijiji, Ofisa Mtendaji wa Kijiji na askari aliyetoa PF3. Amesema watu hao hawakuwa mashahidi muhimu kwa kuwa hakuna ushahidi ulioonyesha kuwa walishuhudia tukio hilo au ushahidi wao ungeongeza ukweli ambao haukuwa umeelezwa na mashahidi waliotoa ushahidi. Kuhusu madai ya Msemo kwamba hakuwa mzima wa akili, Jaji amesema hakuna jambo hilo katika kumbukumbu za kesi lililoonyesha kuwa alikuwa na tatizo hilo na hakukuwa na tabia isiyo ya kawaida iliyorekodiwa wakati wa kesi, hakutoa utetezi wa kichaa na alitoa utetezi wake, hivyo madai hayo hayakuwa na msingi. Jaji amesema baada ya kutathmini upya ushahidi, Mahakama iliridhika kuwa vipengele muhimu vya kosa, ambavyo ni umri wa mwathiriwa, kupenya na utambulisho wa mshtakiwa vilithibitishwa bila shaka yoyote. Hata hivyo, Jaji alibaini kuwa Mahakama ya Wilaya ya Pangani ilikosea katika kutoa adhabu ya kifungo cha miaka 30 badala ya kifungo cha maisha na kuwa mtoto alikuwa na umri wa mwaka mmoja na miezi minne, alikuwa chini ya miaka 10, hivyo kifungu cha 131(3) cha Kanuni ya Adhabu kinataka adhabu ya kifungo cha maisha. “Kwa kuwa sikuona msingi wowote wa rufaa, rufaa hiyo imetupiliwa mbali kabisa. Ninarekebisha hukumu hiyo kwa kubadilisha kifungo cha miaka 30 na kuwa kifungo cha maisha jela ,” amehitimisha Jaji Ndesamburo.

This article was sourced from an external publication.

Share this article
OneClick Africa Logo

Africa's premier digital hub for impactful news, entertainment, and business insights.

© 2026 OneClick Africa. All rights reserved.