TRENDING
Chaumma wamng'oa Mwalimu, Kigaila apewa mikoba
Back to Home

Chaumma wamng'oa Mwalimu, Kigaila apewa mikoba

Mwananchi about 2 hours 1 mins read
Dar es Salaam. Halmashuri Kuu ya Chama cha Ukombozi wa Umma( Chaumma), imemng'oa aliyekuwa katibu mkuu wa chama hicho, Salum Mwalimu huku ikimkaimisha Benson Kigaila kuongoza wadhifa huo. Wajumbe 31 wa halmashauri kuu ya Chaumma kwa kauli moja imepiga kura ya ndio ya kutokuwa na imani na Mwalimu wakimtuhumu kwa makosa mbalimbali ikiwamo ya matumizi mabaya ya ofisi na ubadhirifu wa fedha za chama. Mkurugenzi wa Oganizesheni, Mipango na Uchaguzi, Ismail Kangeta ameliambia Mwananchi leo Juni 30,2026 kuwa kikao kilichomalizika usiku huu ndio kimefikia uamuzi huo. "Tumetengua uteuzi wa Mwalimu, tumemkaimisha Kigaila katika nafasi hiyo," amesema Kangeta. Kabla ya kung'olewa, mapema leo, Mwalimu aliwasilisha barua kwa Mwenyekiti, akiomba kuundwe timu ya kuchunguza tuhuma zinazomkabili na alisema angekuwa tayari kuwa nje ya ofisi kupisha uchunguzi huo. Miongoni mwa sababu zinazotajwa na wajumbe kutokuwa na imani na kiongozi huyo ni matumizi mabaya ya ofisi, kupongeza ushindi wa CCM katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29 na ubadhirifu wa fedha. Endelea kufuatilia Mwananchi…

This article was sourced from an external publication.

Share this article

Comments (0)

Want to join the discussion?

Sign in to post comments and engage with the community.

Be the first to comment!

Innovation

View All

Automobiles

View All

Telecommunications

View All
AD

Information Technology

View All

Science & Technology

View All
OneClick Africa Logo

Africa's premier digital hub for impactful news, entertainment, and business insights.

© 2026 OneClick Africa. All rights reserved.