TRENDING
Sterling Pleads Guilty To Dangerous Driving After Crashing Lamborghini On Motorway • EUROMATCH-NPFL 2026/27: Ayeni Targets Sustained Doma United Surge After Perfect Start • LIFTELLER Is Here: The New Social Platform Using Technology and Compassion to Lift Millions • AGF rallies Kwara varsity stakeholders for greater heights • Nigerian Bottling Company marks 75 years of growing with Nigeria • لليوم الخامس تواليا.. أزمة وقود خانقة تضرب الخرطوم • دقلو يوجه بتوحيد سعر الكاش وبنكك في دارفور • Building Resilient Foundations for Better Health Outcomes, Using the Bottom-to-Top Approach • South Africa secures $1bn NDB loan for municipal infrastructure • AFRICA FINANCE IN BRIEF: Dangote IPO, South Africa’s $1bn loan and rising energy costs dominate • Linkage Assurance targets Nigerians abroad with new diaspora insurance product • Howard Webb says accidental handball law ‘a nonsense’ and calls for reform • Raheem Sterling could face prison for reckless driving while using nitrous oxide • I Back Tinubu For 2027, But PDP Will Contest Other Elections – Wike • مقتل 3 أشخاص في اشتباك بوسط دارفور • Lere Paimo counters Pete Edochie, says he started acting in 1958 • Over 800 farmers to receive compensation for Accra-Kumasi Expressway — Brigadier Jonas Wiafe • Mahama summons security, port agencies to answer major drug seizures linked to Ghana • Sokoto sets up committee to investigate cleric’s controversial remarks against Prophet Muhammad • Seven things to know about the Dangote refinery IPO • Sterling Pleads Guilty To Dangerous Driving After Crashing Lamborghini On Motorway • EUROMATCH-NPFL 2026/27: Ayeni Targets Sustained Doma United Surge After Perfect Start • LIFTELLER Is Here: The New Social Platform Using Technology and Compassion to Lift Millions • AGF rallies Kwara varsity stakeholders for greater heights • Nigerian Bottling Company marks 75 years of growing with Nigeria • لليوم الخامس تواليا.. أزمة وقود خانقة تضرب الخرطوم • دقلو يوجه بتوحيد سعر الكاش وبنكك في دارفور • Building Resilient Foundations for Better Health Outcomes, Using the Bottom-to-Top Approach • South Africa secures $1bn NDB loan for municipal infrastructure • AFRICA FINANCE IN BRIEF: Dangote IPO, South Africa’s $1bn loan and rising energy costs dominate • Linkage Assurance targets Nigerians abroad with new diaspora insurance product • Howard Webb says accidental handball law ‘a nonsense’ and calls for reform • Raheem Sterling could face prison for reckless driving while using nitrous oxide • I Back Tinubu For 2027, But PDP Will Contest Other Elections – Wike • مقتل 3 أشخاص في اشتباك بوسط دارفور • Lere Paimo counters Pete Edochie, says he started acting in 1958 • Over 800 farmers to receive compensation for Accra-Kumasi Expressway — Brigadier Jonas Wiafe • Mahama summons security, port agencies to answer major drug seizures linked to Ghana • Sokoto sets up committee to investigate cleric’s controversial remarks against Prophet Muhammad • Seven things to know about the Dangote refinery IPO
Jamhuri ilivyomhoji Heche kuhusu ‘utajiri’ wake
Back to Home

Jamhuri ilivyomhoji Heche kuhusu ‘utajiri’ wake

Mwananchi 1 day 5 mins read
Dar es Salaam. Jamhuri imehoji umiliki wa mali wa Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Bara, John Heche, ikiwamo magari, chanzo cha kipato na madai ya kupokea fedha kutoka kwa watu mbalimbali. Heche, ambaye ni shahidi wa tano katika kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema, Tundu Lissu, ameingia katika hatua ya kuhojiwa na Jamhuri kuhusu ushahidi alioutoa katika kesi hiyo. Hoja hizo zimeibuliwa leo Jumatatu, Septemba 14, 2026, na Wakili wa Serikali Mkuu, Nassoro Katuga, wakati akimhoji Heche katika Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Dar es Salaam. Katika mahojiano hayo, Katuga amemuuliza Heche kuhusu elimu yake, majina aliyotumia shuleni, ajira na kipato chake, pamoja na mali anazomiliki, hasa magari. Pia amemuuliza kuhusu utaratibu wa Chadema wa kupokea michango kutoka kwa wafanyabiashara, marafiki na wadau wengine, akidai kuwa Heche aliwahi kupokea fedha kutoka kwa mfanyabiashara anayetajwa kwa jina la Nilesh. Heche amekanusha madai hayo, akisema hamfahamu Nilesh na hajawahi kupokea fedha kutoka kwake kwa ajili ya chama. Lissu anakabiliwa na shtaka la uhaini akidaiwa kutenda kosa kinyume na Kifungu cha 39(2)(d) cha Kanuni ya Adhabu (Penal Code), Sura ya 16, kama ilivyorekebishwa mwaka 2022. Anadaiwa kuwa Aprili 3, 2025, akiwa raia wa Tanzania, kwa nia ya uchochezi alishawishi umma kuzuia kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, kwa kutamka na kuchapisha mtandaoni maneno ya kumshinikiza kiongozi mkuu wa Serikali. Maneno hayo, yanayodaiwa kuwa ya uhaini, Lissu alitamka: “Wanasema kitu kimoja hapa, msimamo huu unaashiria uasi, ni kweli..., kwa sababu tunasema tutazuia uchaguzi, tutahamasisha uasi, hivyo ndivyo namna ya kupata mabadiliko..., kwa hiyo tunaenda kukinukisha..., sana sana, huu uchaguzi tutauvuruga kwelikweli..., tunaenda kukinukisha vibaya sana...” Kesi hiyo inasikilizwa na jopo la majaji watatu, Dunstan Ndunguru ambaye ni kiongozi wa jopo, James Karayemaha na Ferdinand Kiwonde, ikiwa katika hatua ya utetezi. Heche alianza kuhojiwa na Jamhuri leo kuhusu ushahidi alioutoa awali. Sehemu ya mahojiano kati yake na Wakili Katuga ilikuwa kama ifuatavyo: Wakili: Shahidi, kwanza nikueleze tu kuwa lengo la mahojiano haya ni kufanya ushahidi wako uonekane wa uongo. Wakili: Waambie majaji una elimu gani? Shahidi: Nina shahada ya elimu. Wakili: Kwa maneno rahisi, wewe ni mwalimu, ni sahihi? Shahidi: Ni sahihi. Wakili: Ni kweli ulipomaliza sekondari ulienda moja kwa moja chuo kikuu? Shahidi: Nilipomaliza kidato cha nne nilienda kuchukua diploma ya ualimu, baadaye nikaenda chuo kikuu kuchukua shahada ya elimu. Wakili: Ni kweli kuanzia shule ya msingi hadi sekondari ulisoma kwa jina la Wegesa Chacha Suguti? Shahidi: Ni kweli. Wakili: Ni kweli kidato cha nne ulipata Division Four ya pointi 26? Shahidi: Nilipata Division One ya pointi 11. Wakili: Unajua kuwa taarifa hizi zinaingia kwenye kumbukumbu za mahakama? Shahidi: Ndiyo. Huwezi kupata Division Four ukaenda Musoma Alliance. Wakili: Tuambie jina la Suguta David Heche ni nani? Shahidi: Ni mdogo wangu. Wakili: Mdogo wako wa ngapi? Shahidi: Nina wadogo zangu watatu. Baba yangu alikuwa na wake wanane. Wakili: Umeiambia mahakama kwamba mbali na cheo chako cha Makamu Mwenyekiti wa Chadema, unajishughulisha na kitu gani kingine? Shahidi: Sijaiambia. Wakili: Umeiambia mahakama kama Makamu Mwenyekiti wa Chadema analipwa mshahara au posho? Shahidi: Sikuiambia. Wakili: Sasa waambie waheshimiwa majaji, kwa cheo chako cha Makamu Mwenyekiti, unalipwa posho au mshahara? Shahidi: Silipwi chochote. Wakili: Waambie waheshimiwa majaji kama ni kweli una malori yanayofanya kazi nchini Kenya. Shahidi: Hapana. Wakili: Waambie waheshimiwa majaji kama ni kweli una magari manne ya bei mbaya. Shahidi: Nina magari mawili, hiyo bei mbaya sijui ndiyo nini. Wakili: Unajua taarifa za magari zinahifadhiwa TRA? Shahidi: Ni sahihi. Baada ya kupata ridhaa ya mahakama, Wakili Katuga alimkabidhi Heche nyaraka mbalimbali zinazohusiana na kadi za magari. Wakili: Ziko ngapi? Shahidi: Kadi zipo tano, siyo zote ni magari, nyingine ni mashine. Wakili: Sikiliza shahidi. Waambie waheshimiwa majaji, umiliki huo ni wa gari za aina gani? Shahidi: Ni trekta kwa ajili ya kilimo cha parachichi, Canter Mitsubishi, Toyota Crown, Harrier Double Cabin na Toyota Prado. Wakili: Waambie majaji, Mitsubishi, Crown na Prado ni magari au siyo magari? Shahidi: Ni magari. Wakili: Haya magari yapo mangapi? Shahidi: Wewe ulisema magari ya bei mbaya. Wakili: Shahidi, jibu swali, yako mangapi? Shahidi: Manne. Wakili: Sasa mbona ulisema mawili? Hapa tunaanza kukujua wewe ni nani, kama unaishi katika unayoyaongea au unaishiishi tu. Katuga kisha aliendelea na maswali kuhusu utaratibu wa Chadema wa kupokea fedha. Wakili: Utaratibu wa Chadema, kiongozi au mwenyekiti anapopokea fedha za michango kwa ajili ya chama kutoka kwa marafiki, wafanyabiashara au watu wa Ulaya, huwa anafanya nini? Shahidi: Nitapokea vipi fedha? Pesa huwa zinapokelewa na Katibu Mkuu. Wakili: Zile pesa ulizopokea kutoka kwa Nilesh, ulipeleka wapi? Shahidi: Mimi simjui, kwa hiyo sijapokea pesa kwa mtu ambaye simjui. Wakili: Ukiletwa uthibitisho hapa utasemaje? Shahidi: Lete. Wakili: Kuna mtu anaitwa Salman, unamfahamu? Shahidi: Simfahamu. Wakili: Ni kweli alikuingizia kwenye akaunti yako Sh10 milioni na baadaye Sh20 milioni? Shahidi: Siyo kweli. Wakili: Baada ya Salman kukuingizia hizo pesa ulipeleka wapi? Shahidi: Simfahamu mtu anayeitwa Salman. Wakili: Nakuonyesha hizi risiti. Ni kweli una akaunti Benki ya CRDB? Shahidi: Ni sahihi. Wakili: Ni kweli hii ndiyo akaunti yako? Shahidi: Ni sahihi. Wakili: Kwa hiyo ni kweli, kwa mujibu wa risiti hizo, alikuingizia Sh30 milioni kwenye akaunti yako? Shahidi: Ni kweli. Wakili: Ni kweli, kwa mujibu wa risiti hiyo, fedha ziliingizwa na zipo katika akaunti yako? Shahidi: Ni kweli. Shahidi huyo bado anaendelea kuhojiwa na waendesha mashtaka. Endelea kufuatilia Mwananchi

This article was sourced from an external publication.

Share this article
OneClick Africa Logo

Africa's premier digital hub for impactful news, entertainment, and business insights.

© 2026 OneClick Africa. All rights reserved.