TRENDING
#OsunDecides2026: Observers record 323 irregularities, 38 security incidents • Osun Election: Adeleke condemns arrest of Osun PDP chair, demands release • UK reveals how much money you must declare when entering Britain • Police nab 27-year-old over fatal hotel stabbing in Adamawa • (UPDATED)#OsunDecides2026: INEC uploads 1,340 of 3,763 Osun election results • BREAKING: Osun decides: INEC uploads 37 per cent of election results to IReV • JUST IN: #OsunDecides2026: APC’s founding chair, former Osun governor Bisi Akande wins polling unit • Osun decides: INEC uploads 37 per cent of election results to IReV • Davido questions delay in uploading Osun Governorship results to IReV Portal • ‘I Am Not Satisfied’: Adeleke slams BIVAS delays and security lapses • Oyo police command nab 10 suspected human parts merchants, recover human parts, charms • Middlesbrough 2-1 Lincoln, Bristol City 0-2 Millwall, Norwich 1-2 West Brom: football - as it happened • Prayers will crush Boko Haram, Borno Catholic bishop says • At least 47 dead in eastern Indonesian earthquake • Sokoto Tasks Corps Members to Drive Local Devt • Chiana-Paga MP donates GH¢14,000 to support Kazugu community CHPS compound • GWJN urges Journalists to prioritize accuracy, balance, and community voices • Bayelsa Most Polluted State in Nigeria, Says Environmentalist, Nnimmo Bassey • WN/R: 21 travellers escape death in Lineso Barrier crash • Government releases GH¢443 million for Free Primary Health Care — NHIA CEO • #OsunDecides2026: Observers record 323 irregularities, 38 security incidents • Osun Election: Adeleke condemns arrest of Osun PDP chair, demands release • UK reveals how much money you must declare when entering Britain • Police nab 27-year-old over fatal hotel stabbing in Adamawa • (UPDATED)#OsunDecides2026: INEC uploads 1,340 of 3,763 Osun election results • BREAKING: Osun decides: INEC uploads 37 per cent of election results to IReV • JUST IN: #OsunDecides2026: APC’s founding chair, former Osun governor Bisi Akande wins polling unit • Osun decides: INEC uploads 37 per cent of election results to IReV • Davido questions delay in uploading Osun Governorship results to IReV Portal • ‘I Am Not Satisfied’: Adeleke slams BIVAS delays and security lapses • Oyo police command nab 10 suspected human parts merchants, recover human parts, charms • Middlesbrough 2-1 Lincoln, Bristol City 0-2 Millwall, Norwich 1-2 West Brom: football - as it happened • Prayers will crush Boko Haram, Borno Catholic bishop says • At least 47 dead in eastern Indonesian earthquake • Sokoto Tasks Corps Members to Drive Local Devt • Chiana-Paga MP donates GH¢14,000 to support Kazugu community CHPS compound • GWJN urges Journalists to prioritize accuracy, balance, and community voices • Bayelsa Most Polluted State in Nigeria, Says Environmentalist, Nnimmo Bassey • WN/R: 21 travellers escape death in Lineso Barrier crash • Government releases GH¢443 million for Free Primary Health Care — NHIA CEO
Sh11 bilioni kujenga kituo cha saratani Mbeya
Back to Home

Sh11 bilioni kujenga kituo cha saratani Mbeya

Mwananchi about 1 hour 4 mins read
Mbeya. Serikali imetoa Sh11 bilioni kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Saratani katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya (MZRH), huku watu 30,000 wakiripotiwa kufariki dunia nchini kati ya wagonjwa 45,000 wanaobainika kuwa na ugonjwa huo. Uwekezaji huo unalenga kusogeza huduma za saratani karibu na wananchi wa Nyanda za Juu Kusini, kupunguza gharama na adha ya kusafiri umbali mrefu kufuata matibabu, pamoja na kutoa fursa kwa wagonjwa kutoka nchi jirani kupata huduma hizo Mbeya. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road, Dk. Diwani Msemo, amesema hayo leo, Jumamosi, Agosti 15, 2026, wakati wajumbe wa kamati ya bodi walipotembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa kituo hicho katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya. Amesema ujenzi wa kituo hicho ni sehemu ya mkakati wa Serikali wa kusambaza huduma za kibingwa na kibobezi katika maeneo mbalimbali nchini. “Katika mkakati wa Serikali wa kupambana na saratani wa mwaka 2012 wa kipindi cha miaka 10, Taasisi ya Ocean Road ilipewa jukumu la kusambaza huduma za kibingwa na kibobezi nchini, sambamba na kuwa na mpango kazi wa kuhakikisha huduma zinafika maeneo mbalimbali,” amesema. Amesema baada ya kituo cha Mbeya, Serikali inapanga kujenga vituo vingine Arusha, Kigoma na Mtwara, ambako tayari maeneo kwa ajili ya uwekezaji yamepatikana. Dk Msemo amesema Sh11 bilioni zilizotolewa hadi sasa zimetumika katika ujenzi wa kituo hicho, huku gharama ya uwekezaji ikitarajiwa kufikia zaidi ya Sh30 bilioni baada ya kukamilika kwa ufungaji wa mashine na vifaa vingine. Amesema Serikali imewekeza zaidi ya Sh60 bilioni katika Taasisi ya Saratani Ocean Road kwa ajili ya kuboresha miundombinu na huduma. “Sh11 bilioni zimetumika kwa ajili ya ujenzi pekee, lakini bado kuna hatua ya ufungaji wa mashine na vitu vingine, hivyo uwekezaji wote utafikia zaidi ya Sh30 bilioni,” amesema. Amesema maendeleo ya ujenzi yanaendelea vizuri na bodi ya taasisi hiyo imeridhishwa na hatua iliyofikiwa, huku kituo hicho kikitarajiwa kukamilika Januari 2027. “Lengo ni ifikapo Januari 2027 kituo kikamilike na wananchi wa Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini waanze kunufaika na huduma,” amesema. Dk Msemo amesema kituo hicho pia kitachochea utalii wa tiba kutokana na wagonjwa kutoka Zambia, Malawi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) kupata huduma Mbeya badala ya kusafiri hadi Ocean Road jijini Dar es Salaam. Amesema hali hiyo itasaidia kupunguza gharama kwa wagonjwa kutoka nchi hizo ambao wamekuwa wakitumia fedha nyingi kusafiri umbali mrefu kufuata huduma za saratani. Akizungumzia hali ya saratani nchini, Dk Msemo amesema bado ni changamoto kubwa, akisema takwimu zinaonesha wagonjwa 45,000 hubainika kuwa na saratani nchini, huku 30,000 kati yao wakifariki dunia. Amesema kwa mujibu wa takwimu za dunia za mwaka 2024, watu milioni 20 walibainika kuwa na saratani, huku milioni 9.7 wakifariki kutokana na ugonjwa huo. “Kwa Tanzania, watu 45,000 hubainika kuwa na saratani, kati yao 30,000 hupoteza maisha. Kwa maana nyingine, kila saa mtu mmoja hufariki kutokana na saratani,” amesema. Hata hivyo, amesema takribani asilimia 50 ya saratani zinaweza kuzuilika na nyingine kugundulika katika hatua za awali, jambo linalosisitiza umuhimu wa uwekezaji katika uchunguzi na matibabu. Mkurugenzi wa Tiba kutoka Wizara ya Afya, Hamad Nyembea, amesema Serikali imeamua kuwekeza katika huduma bobezi ili kupunguza gharama na adha kwa wananchi wanaosafiri umbali mrefu kufuata matibabu ya saratani. “Nyanda za Juu Kusini wagonjwa walikuwa wakisafiri kwenda Taasisi ya Ocean Road kupata huduma za saratani, lakini Serikali, baada ya kuliona hilo, imesogeza huduma na kujenga kituo hiki ambacho tunatarajia kukamilisha Januari 2027,” amesema. Amesema Serikali ina mpango mkubwa wa kutekeleza miradi mingine katika Ukanda wa Kusini na maeneo mengine nchini ifikapo mwaka 2030, ili kuhakikisha huduma za saratani zinapatikana kwa uhakika na kuwafikia wananchi kwa wakati. Akizungumza kwa niaba ya wananchi, Mjumbe wa Bodi ya Taasisi ya Saratani Ocean Road, Aisha Kwegia amesema uwepo wa kituo hicho katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini utawasaidia wananchi kupata huduma za saratani karibu na maeneo yao. Amesema hatua hiyo itapunguza adha iliyokuwepo awali, wagonjwa walilazimika kusafiri hadi Dar es Salaam kufuata huduma hizo.

This article was sourced from an external publication.

Share this article
OneClick Africa Logo

Africa's premier digital hub for impactful news, entertainment, and business insights.

© 2026 OneClick Africa. All rights reserved.