TRENDING
SMZ yaeleza kutoridhishwa na mkandarasi ZTT, kuchukua hatua za kisheria
Back to Home

SMZ yaeleza kutoridhishwa na mkandarasi ZTT, kuchukua hatua za kisheria

Mwananchi about 2 hours 3 mins read
Unguja. Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Hemed Suleiman Abdulla amesema haridhishwi na utendaji kazi wa Kampuni ya ZTT iliyopewa kazi ya kujenga laini za kusambaza umeme. Kutokana na uhitaji mkubwa wa huduma ya nishati ya umeme Zanzibar, ameuagiza uongozi wa Wizara ya Maji, Nishati na Madini kukaa pamoja na wafadhili wa mradi huo, Benki ya Dunia (WB), ili kuangalia namna bora ya kuitafutia ufumbuzi changamoto ya kuchelewa kukamilika kwa miradi inayotekelezwa na ZTT. Hemed ametoa kauli hiyo leo Julai 16, 2026 baada ya kukagua ujenzi wa mradi wa kituo cha kupokea na kutoa nishati ya Umeme Welezo na kukagua ukarabati wa majenereta ya uzalishaji wa umeme yaliyopo Mtoni Wilaya ya Magharibi A Unguja. Amesema kasi ya ujenzi wa miradi inayotekelezwa na kampuni ya ZTT hairidhishi na imesababisha kuchelewa kukamilika kwa miradi hiyo. “Hatua hiyo inasababisha hasara kwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) na kuleta usumbufu kwa wananchi wanaotegemea kupata huduma kupitia miradi hiyo,” amesema. Mtendaji mkuu huyo wa SMZ, amesema Serikali inatekeleza miradi mikubwa ya maendeleo ikiwemo bandari, viwanja vya ndege na barabara ili kuimarisha uwekezaji na kujenga uchumi imara, ambapo miradi yote hiyo inahitaji umeme wa uhakika. Akikagua kituo cha kupokelea umeme Mtoni, Hemed amelipongeza Shirika la Umeme Zanzibar (Zeco) kuona umuhimu wa kuyafanyia matengenezo majenerata 30 na kuyawekea mifumo ya kisasa, ambayo hutambua maeneo yenye uhaba wa umeme na kusaidia kutatua changamoto hiyo kwa haraka. Amesema kutengamaa kwa majenereta hayo yanayozalisha umeme wa megawati 20, inaonyesha wazi dhamira ya dhati ya Zeco ya kuona Zanzibar inaondokana na changamoto ya uhaba wa umeme. Ametumia fursa hiyo kuwapongeza wananchi kuendelea kuwa wavumilivu katika kipindi hiki Zanzibar ikiendelea na ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo. Naye, Waziri wa Maji, Nishati na Madini, Nadir Abdullatif Alwardy amesema ifikapo mwaka 2030, Zanzibar haikutakuwapo changamoto ya upatikanaji umeme kutokana na juhudi zinazochukuliwa sasa. Kuhusu kampuni ya ZTT, amesema wizara yake imejipanga kuichukulia hatua za kisheria kutokana na kutokamilisha miradi kwa wakati na kuisababishia Serikali hasara kubwa huku wananchi wakikosa huduma ya umeme inayohitajika. Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Zeco, Haji Haji amesema mradi wa kituo cha kupokea na kutoa umeme Welezo ni miongoni mwa miradi mitatu inayofadhiliwa na WB inayojengwa kwa gharama ya zaidi ya Sh59 bilioni na unatarajiwa kukamilika Novemba 2026. “Mradi huu umefikia asilimia 75 ya ujenzi ambapo changamoto kubwa inayotukabili kwa sasa ni miradi itakapokamilika itashindwa kufanya majaribio kutokana na ZTT kushindwa kukamilisha ujenzi wa laini za kusambazia umeme,” amesema. Hata hivyo, uongozi wa kampuni ya ZTT haukuwa tayari kuzungumza na waandishi wa habari kuhusu changamoto hiyo.

This article was sourced from an external publication.

Share this article

Comments (0)

Be the first to comment!

DR Congo

View All

Senegal

View All
AD

Traditional Affairs

View All

Somalia

View All
AD
OneClick Africa Logo

Africa's premier digital hub for impactful news, entertainment, and business insights.

© 2026 OneClick Africa. All rights reserved.