TRENDING
Tinubu Mourns Elder Statesman, Bamanga Tukur • Breaking: Bamanga Tukur is Dead • Nigeria’s Patience Wearing Thin Over Killings in South Africa, Fani-Kayode • Benue still bleeding – Peter Obi laments latest attack • Suspected alcohol poisoning: Ondo activates multi-agency investigation team as death toll rises • 2027: Jonathan’s ex-spokesperson joins Tinubu’s campaign council • How my father’s investments saved me after I went bankrupt at 27 — Daniel Amokachi • JKT kutumika kukamata watupa taka ovyo Dar • Sita wafariki ajali ya Hiace Kilimanjaro, tisa wajeruhiwa • Bamanga Tukur, former Adamawa gov, ex-PDP Chair dies • INEC unveils final list of presidential candidates for 2027 election • Ondo govt links naming ceremonies to 29 deaths from ” Monkey Tail” consumption • Tinubu Felicitates Katsina Gov, Etsu Nupe on 57th, 74th Birthdays • AGCOMS Launches Academy to Tackle Skills Gap in Nigeria’s Mechanisation Drive • ANALYSIS: Taraba 2027: Kefas, Bwacha, others and the battle ahead • 2027: Political chameleon, veteran presidential candidate – Presidency hits Atiku • ‘We must remove criminals from Southwest’ – Igboho tells Iru Ekun volunteers • FG condemns killing of two Nigerians in South Africa, demands probe • Sources: Raiders TE Mayer lands $45M extension as Bowers sidelined • Just in: Bamanga Tukur, former Adamawa Gov, dies • Tinubu Mourns Elder Statesman, Bamanga Tukur • Breaking: Bamanga Tukur is Dead • Nigeria’s Patience Wearing Thin Over Killings in South Africa, Fani-Kayode • Benue still bleeding – Peter Obi laments latest attack • Suspected alcohol poisoning: Ondo activates multi-agency investigation team as death toll rises • 2027: Jonathan’s ex-spokesperson joins Tinubu’s campaign council • How my father’s investments saved me after I went bankrupt at 27 — Daniel Amokachi • JKT kutumika kukamata watupa taka ovyo Dar • Sita wafariki ajali ya Hiace Kilimanjaro, tisa wajeruhiwa • Bamanga Tukur, former Adamawa gov, ex-PDP Chair dies • INEC unveils final list of presidential candidates for 2027 election • Ondo govt links naming ceremonies to 29 deaths from ” Monkey Tail” consumption • Tinubu Felicitates Katsina Gov, Etsu Nupe on 57th, 74th Birthdays • AGCOMS Launches Academy to Tackle Skills Gap in Nigeria’s Mechanisation Drive • ANALYSIS: Taraba 2027: Kefas, Bwacha, others and the battle ahead • 2027: Political chameleon, veteran presidential candidate – Presidency hits Atiku • ‘We must remove criminals from Southwest’ – Igboho tells Iru Ekun volunteers • FG condemns killing of two Nigerians in South Africa, demands probe • Sources: Raiders TE Mayer lands $45M extension as Bowers sidelined • Just in: Bamanga Tukur, former Adamawa Gov, dies
Tanzania yachangamkia fursa ushirikiano wa teknolojia Korea
Back to Home

Tanzania yachangamkia fursa ushirikiano wa teknolojia Korea

Mwananchi about 2 hours 4 mins read
Seoul, Korea Kusini. Tanzania imeanza kuweka mkazo katika kupata ujuzi na teknolojia kutoka Korea Kusini, ikilenga kutumia ushirikiano wa vyuo vikuu na sekta binafsi kujenga kizazi cha vijana wenye uwezo wa kushindana katika uchumi wa kidijitali. Hatua hiyo imeibuliwa baada ya ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Waziri wa Fedha, Khamis Mussa Omar, kutembelea Chuo Kikuu cha Hanyang ERICA jijini Seoul, pembezoni mwa Mkutano wa Mawaziri wa Jukwaa la Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Korea na nchi za Afrika (KOAFEC). Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Angellah Kairuki, ambaye ameambatana na Waziri Omar, amesema Tanzania inahitaji kubadili ushirikiano wa kimataifa kutoka kwenye makubaliano ya kawaida na kuufanya uwe chanzo cha ujuzi, ubunifu na teknolojia zitakazogusa maisha ya wananchi. Amesema matumizi ya Akili Unde (AI) na mabadiliko ya kidijitali ni miongoni mwa maeneo muhimu ambayo Tanzania inapaswa kuyawekea mkazo ili kutimiza malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. “Tunataka kuona matokeo ya haraka katika mafunzo ya rasilimali watu, ujenzi wa maabara na kuanzishwa kwa kampuni changa (startups),” amesema. Kairuki amependekeza hatua tisa za kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Hanyang ERICA, zikiwamo utiaji saini wa hati ya makubaliano (MOU), kubadilishana wanafunzi na mafunzo kwa wahadhiri. Pendekezo jingine ni kuanzishwa kwa Korea-Tanzania Digital Innovation Lab, kituo cha pamoja kitakacholenga utafiti, ubunifu na matumizi ya teknolojia katika kutatua changamoto za maendeleo. Ushirikiano huo unaweza kuwa na umuhimu mkubwa katika kuongeza idadi ya wataalamu wenye ujuzi wa AI, sayansi ya data, roboti, usalama wa mtandao na teknolojia ya semikondakta, maeneo ambayo yanazidi kuwa muhimu katika uchumi wa dunia. Kairuki amesema ERICA ina uwezo wa kutekeleza mapendekezo hayo na kuitaka taasisi hiyo kuangalia namna ya kuanza utekelezaji wa maeneo ambayo yanaweza kuzaa matokeo kwa muda mfupi. Ameialika pia menejimenti ya Hanyang ERICA, akiwemo Makamu wa Rais wa chuo hicho, Profesa Dong Baek, kutembelea Tanzania kwa ajili ya kuona fursa zilizopo katika sekta mbalimbali za uchumi na uwekezaji. Amesema ziara hiyo itatoa nafasi kwa ujumbe huo kutembelea Dodoma, Dar es Salaam na Zanzibar na kuona kwa vitendo mazingira ya Tanzania katika kutumia teknolojia na fursa za uwekezaji. Akijibu mapendekezo hayo, Profesa Baek amesema yana umuhimu na kwamba baadhi yake yanaweza kuanza kutekelezwa bila vikwazo vikubwa. Amesema Serikali ya Korea tayari imetenga fedha kwa ajili ya ushirikiano na Tanzania, jambo ambalo linaweza kusaidia kuwezesha baadhi ya miradi inayopendekezwa. Ameahidi kuwa chuo hicho kitayapitia mapendekezo hayo kwa kina na kutafuta njia bora za kuyatekeleza. Kwa upande wake Waziri Omar amesema Tanzania imejipanga kuendeleza ushirikiano kati yake na Hanyang ERICA. Ziara hiyo inakuja wakati Serikali ikiweka msisitizo katika matumizi ya teknolojia na ubunifu kama sehemu ya maandalizi ya uchumi unaozingatia maarifa. Kwa nini Hanyang ERICA? Hanyang ERICA ni chuo kinachoweka mkazo mkubwa katika utafiti na teknolojia, kikiwa na utaalamu katika maeneo kama AI, sayansi ya data, roboti, usalama wa mtandao na semikondakta. Chuo hicho pia kinatumia mfumo wa Industry-Coupled Problem-Based Learning (ICPBL) unaowaunganisha wanafunzi na changamoto halisi zinazotokana na sekta ya viwanda. Mfumo huo unalenga kuwafanya wanafunzi wasibaki na maarifa ya darasani pekee, bali wayatumie katika kutengeneza suluhisho zinazoweza kutumiwa na viwanda na jamii. Chuo hicho pia kinafanya kazi kwa karibu na sekta ya teknolojia na viwanda, kikiwa na miundombinu kama Campus Innovation Park na Ansan Science Valley. Kwa Tanzania, uzoefu huo unaweza kuwa muhimu katika kuimarisha uhusiano kati ya vyuo vikuu, utafiti na mahitaji ya soko la ajira. Ujuzi kwa vijana Iwapo mapendekezo hayo yatatekelezwa, wanafunzi na watafiti wa Tanzania wanaweza kupata nafasi zaidi za mafunzo, utafiti wa pamoja na kubadilishana uzoefu na wenzao wa Korea. Vilevile, kuanzishwa kwa kituo cha pamoja cha ubunifu kunaweza kutoa nafasi kwa vijana wenye mawazo ya kiteknolojia kuyageuza kuwa bidhaa na huduma kupitia kampuni changa.

This article was sourced from an external publication.

Share this article
OneClick Africa Logo

Africa's premier digital hub for impactful news, entertainment, and business insights.

© 2026 OneClick Africa. All rights reserved.