TRENDING
Wadudu wachavushaji kuwakutanisha wadau Tanzania
Back to Home

Wadudu wachavushaji kuwakutanisha wadau Tanzania

Mwananchi about 3 hours 3 mins read
Arusha. Zaidi ya wadau 1,000 wa kilimo, biashara, uhifadhi wa mazingira na teknolojia 1000 kutoka nchi za Afrika wanatarajiwa kukutana nchini Kwa siku tatu kujadili namna ya kulinda wadudu wachavushaji, kuongeza uzalishaji wa mazao na kuimarisha uchumi wa kilimo kupitia teknolojia za kisasa. Mkutano huo wa kwanza wa uchavushaji mimea Afrika (Pollination Africa Summit), unaotarajia kufanyika septemba 29 hadi octoba 1, 2026 jijini Arusha, unalenga kujadili mustakabali wa uchavushaji wa mazao na usalama wa chakula katika ukanda mzima. Mkutano huo unaoandaliwa na Shirika la Mpango wa Maendeleo Endelevu ya Kilimo na Biashara ya Kilimo Tanzania (SAADIT), kwa ushirikiano na Jumuiya ya Kijani ya Vijijini (GRC), Suluhisho Bunifu za Jamii (ICS), Wakfu wa Dunia Endelevu (SEF) na wafanyakazi wa nyuki Tanzania na Afrika wataweka pia mikakati ya urejelezaji wa bioanuwai katika maeneo tengefu ya Kilimo. Akizungumza kuhusu maandalizi ya mkutano huo, leo Julai 6, 2026 jijini Arusha, Mkurugenzi na Mwanzilishi wa SAADIT, Malulu Martin Igobeko amesema kupungua kwa idadi ya wadudu wachavushaji kutokana na uharibifu wa mazingira na matumizi holela ya viuatilifu kunatishia uzalishaji wa mazao barani Afrika hivyo mkutano huo inalenga kutafuta suluhu ya haraka kabla kukabwa na baa la njaa . Amesema bila wadudu hao, wakiwemo nyuki, mifumo ya uzalishaji wa chakula itaathirika kwa kiwango kikubwa na kuwataka serikali, sekta binafsi na washirika wa maendeleo kuingiza uhifadhi wa wachavushaji katika sera na mipango ya maendeleo ya kitaifa. "Uchavushaji ni msingi wa uzalishaji wa mazao mengi ya chakula. Kulinda wachavushaji ni kulinda usalama wa chakula, kuongeza mavuno na kuimarisha uchumi wa kilimo barani Afrika," alisema. Mjumbe wa Sekretarieti ya Pollination Africa Summit kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara, Genya Charles amesema mkutano huo utajadili pia nafasi ya uchavushaji katika kukuza biashara na uwekezaji kupitia dhana ya uchumi wa uchavushaji. Amesema huduma za uchavushaji zina mchango mkubwa katika kuongeza thamani ya mazao, kuimarisha ushindani wa bidhaa za Afrika katika soko la kimataifa na kufungua fursa mpya za biashara zinazozingatia uchumi wa kijani. Naye, Mercy Butta kutoka Idara ya Usalama wa Chakula katika Wizara ya Kilimo, amesema mafanikio ya Tanzania katika kuwa na ziada ya chakula kwa miaka mingi yanachangiwa kwa kiasi kikubwa na mchango wa nyuki katika uchavushaji wa mazao. Amesema kulinda wadudu hao kutasaidia kuongeza uzalishaji wa mazao na kuinua kipato cha wakulima. Katika mkutano huo, kampuni ya kimataifa ya teknolojia ya ufugaji nyuki kutoka Australia, BeeSTAR Technology, itaonyesha teknolojia za kisasa zinazotumia akili bandia (AI) kufuatilia afya ya mizinga, kuongeza uzalishaji wa asali na kuboresha huduma za uchavushaji wa mazao. Kwa upande wake, Steven Makule wa Innovative Community Solutions, amesema mkutano huo utatoa jukwaa la kuunganisha wataalamu, watafiti, wakulima, wawekezaji na watunga sera kujenga mifumo imara ya kilimo inayoweza kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi. Amesema siku ya kwanza ya mkutano itajikita katika ushahidi wa kisayansi kuhusu umuhimu wa uchavushaji, siku ya pili itaangazia matumizi ya akili bandia na teknolojia za kilimo cha kisasa, huku siku ya mwisho ikihusisha majadiliano ya sera, uwekezaji na ushirikiano wa kikanda.

This article was sourced from an external publication.

Share this article

Comments (0)

Want to join the discussion?

Sign in to post comments and engage with the community.

Be the first to comment!

DR Congo

View All
AD

Senegal

View All

Traditional Affairs

View All
AD

Somalia

View All
OneClick Africa Logo

Africa's premier digital hub for impactful news, entertainment, and business insights.

© 2026 OneClick Africa. All rights reserved.