TRENDING
Wizara ya Afya yawapa ‘kibarua’ wanasayansi
Back to Home

Wizara ya Afya yawapa ‘kibarua’ wanasayansi

Mwananchi about 2 hours 2 mins read
Morogoro. Mkurugenzi wa Maendeleo ya Rasilimali Watu kutoka Wizara ya Afya, Dk Saitore Laizer amesisitiza umuhimu wa kuwakutanisha wanasayansi, watafiti na wataalamu wa sekta mbalimbali ili kujadili masuala ya kisayansi yatakayochangia kupatikana kwa suluhisho, bunifu na kuboresha huduma za afya nchini. Dk Laizer ametoa kauli hiyo leo Alhamisi, Juni 25, 2026, wakati akifungua kongamano la Tano la Kisayansi la Chuo cha Sayansi za Afya cha Mtakatifu Fransisko Ifakara (SFUCHAS), linalolenga kuchochea mafanikio katika kufikia Lengo la Tatu la Maendeleo Endelevu (SDG 3) kupitia ujumuishaji wa tafiti, teknolojia na suluhisho za afya zinazotokana na jamii. Akizungumza katika kongamano hilo, Dk Laizer amesema mijadala ya kisayansi inayowakutanisha wataalamu kutoka nyanja mbalimbali ni muhimu katika kutafuta majibu ya changamoto zinazoikabili sekta ya afya na jamii kwa ujumla. “Nasisitiza umuhimu wa kuendelea kuwa mstari wa mbele katika kuwakutanisha wanasayansi, watafiti na wataalamu mbalimbali kwa lengo la kujadili masuala ya kisayansi yatakayosaidia kuibua suluhisho bunifu katika kuboresha huduma za afya nchini,” amesema. Aidha, ameipongeza SFUCHAS kwa kuendelea kuandaa makongamano ya kisayansi na kuitaka kuongeza wigo wa shughuli hizo ili kufikia kiwango kikubwa zaidi cha kitaifa. Amesema makongamano hayo yana mchango mkubwa katika kutambua changamoto mbalimbali zinazoikabili jamii na kusaidia kupatikana kwa njia bora za kuzitatua kupitia tafiti na ubunifu. Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, Dunstan Kyobya ameiomba Serikali kuangalia uwezekano wa kukipa SFUCHAS hadhi ya kuwa chuo kikuu huru cha afya kutokana na mchango wake katika utoaji wa elimu ya afya na ongezeko la mahitaji ya huduma zake za elimu. Kyobya amesema idadi ya wanafunzi wanaojiunga na chuo hicho kutoka maeneo mbalimbali ya nchi imekuwa ikiongezeka, jambo linaloonyesha umuhimu wake katika kuzalisha wataalamu wa afya wanaohitajika nchini. Pia amekipongeza kwa kushirikiana na wadau mbalimbali katika kuandaa kongamano hilo, akieleza kuwa limekuwa jukwaa muhimu la kuwakutanisha wataalamu wa afya, watafiti na wanasayansi kwa ajili ya kubadilishana uzoefu na maarifa.

This article was sourced from an external publication.

Share this article

Comments (0)

Want to join the discussion?

Sign in to post comments and engage with the community.

Be the first to comment!

Somalia

View All

Senegal

View All
AD

DR Congo

View All
AD

Traditional Affairs

View All
OneClick Africa Logo

Africa's premier digital hub for impactful news, entertainment, and business insights.

© 2026 OneClick Africa. All rights reserved.