TRENDING
Age shouldn’t decide who governs Bayelsa; competence should — Mienye • My dream collaboration is with Rihanna – Davido • Police arrest suspected cultists in Delta community, recover guns • Reps Deputy Speaker Kalu has no business beefing Gov Alex Otti – Aisha Yesufu • US strike cuts water supply in Iran, Iran damages water supply in Kuwait • NCCE Storms 13 Yunyoo Communities With Massive Adolescent Health & Gender Equality Campaign • ICEDEG Africa Presents Recommendations to Finance Ministry Ahead of Mid-Year Budget Review • D’Tigers Assistant Captain Targets World Cup Place, Seeks To Uncover Basketball Talents • Photos: Burna Boy reunites with Shakira ahead of World Cup final halftime show • US places 23 countries on highest ‘do not travel’ alert [FULL LIST] • PFIPC: No legal or factual basis to demand Gbajabiamila’s resignation — Jiti Ogunye • NPFL: Ojokojo appointed Kwara United chief coach • Afenyo‑Markin Calls for Legal Literacy Among Emerging Leaders at Legal Edge Summit • School abduction: Oyo Govt don’t need UN to probe incident – Adewole Adebayo • President Ruto's official website down in second suspected hack within a year • ‘It’s political fight back’ – Sam Amadi on war against corruption in Nigeria • Hart, Rooney and Richards on rowing the Hudson and if Tuchel should keep his job • Gianni Infantino unlikely to face IOC sanctions over Balogun red card scandal • FG Targets 25 Million Tonnes Annual Grain Output • Badejo-Okusanya takes early lead in NBA presidential poll • Age shouldn’t decide who governs Bayelsa; competence should — Mienye • My dream collaboration is with Rihanna – Davido • Police arrest suspected cultists in Delta community, recover guns • Reps Deputy Speaker Kalu has no business beefing Gov Alex Otti – Aisha Yesufu • US strike cuts water supply in Iran, Iran damages water supply in Kuwait • NCCE Storms 13 Yunyoo Communities With Massive Adolescent Health & Gender Equality Campaign • ICEDEG Africa Presents Recommendations to Finance Ministry Ahead of Mid-Year Budget Review • D’Tigers Assistant Captain Targets World Cup Place, Seeks To Uncover Basketball Talents • Photos: Burna Boy reunites with Shakira ahead of World Cup final halftime show • US places 23 countries on highest ‘do not travel’ alert [FULL LIST] • PFIPC: No legal or factual basis to demand Gbajabiamila’s resignation — Jiti Ogunye • NPFL: Ojokojo appointed Kwara United chief coach • Afenyo‑Markin Calls for Legal Literacy Among Emerging Leaders at Legal Edge Summit • School abduction: Oyo Govt don’t need UN to probe incident – Adewole Adebayo • President Ruto's official website down in second suspected hack within a year • ‘It’s political fight back’ – Sam Amadi on war against corruption in Nigeria • Hart, Rooney and Richards on rowing the Hudson and if Tuchel should keep his job • Gianni Infantino unlikely to face IOC sanctions over Balogun red card scandal • FG Targets 25 Million Tonnes Annual Grain Output • Badejo-Okusanya takes early lead in NBA presidential poll
Hoja kukosekana mkalimani wa Kisukuma yashindwa kumnusuru kifungo cha miaka 30
Back to Home

Hoja kukosekana mkalimani wa Kisukuma yashindwa kumnusuru kifungo cha miaka 30

Mwananchi about 2 hours 4 mins read
Arusha. Komanya Makoye, aliyekuwa akipinga kifungo cha miaka 30 jela kwa kosa la ubakaji akidai Mahakama ya Wilaya ya Musoma ilimnyima mkalimani wa lugha ya Kisukuma kwa kuwa hakuelewa Kiswahili, ameshindwa katika hoja hiyo baada ya Mahakama Kuu kubaini kumbukumbu za kesi zinaonyesha alijibu mashtaka yote kwa Kiswahili bila kuonyesha kuwa alikuwa na tatizo la kuelewa mwenendo wa kesi. Mahakama ilibaini kuwa Makoye aliwauliza mashahidi maswali kwa Kiswahili na alijitetea na kujibu maswali yote bila kuonyesha kuwa hakuelewa kilichokuwa kinaendelea mahakamani. Aidha, Mahakama ilitupilia mbali madai ya Makoye kuwa kesi hiyo ilitokana na mgogoro wa deni la Sh milioni mbili kati yake na baba wa mwathiriwa, ikieleza kuwa utetezi huo ulizingatiwa na Mahakama ya Wilaya, lakini haukuibua shaka yoyote dhidi ya ushahidi wa upande wa mashtaka uliomhusisha na kosa la ubakaji. Uamuzi huo ulitolewa Julai 13, 2026 na Jaji Kamazima Kafanabo wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Musoma, wakati akiamua rufaa ya Makoye, akipinga hukumu ya Mahakama ya Wilaya ya Musoma. Katika uamuzi huo, Jaji alithibitisha hukumu ya kifungo cha miaka 30 jela kwa kosa la ubakaji, lakini akafuta hatia na adhabu ya miaka mitano kwa kosa la kumpa mimba mwanafunzi baada ya kubaini shtaka hilo halikuthibitishwa bila kuacha shaka. Kesi ya msingi Kwa mujibu wa ushahidi uliowasilishwa mahakamani katika Mahakama ya Wilaya, ilidaiwa kuwa kati ya Januari na Septemba 2025 katika Kijiji cha Kwibara, Wilaya ya Musoma mkoani Mara, Makoye alifanya ngono mara kadhaa na mwanafunzi huyo aliyekuwa na umri wa miaka 16, ambaye baadaye aligundulika kuwa na ujauzito. Baada ya kutiwa hatiani, Mahakama ya Wilaya ilimhukumu kifungo cha miaka 30 jela kwa kosa la ubakaji na miaka mitano jela kwa kosa la kumpa mimba mwanafunzi, huku adhabu hizo zikienda kwa pamoja. Rufaa Makoye hakuridhika na hukumu hiyo na kukata rufaa akitoa sababu saba, zikiwemo madai kuwa alihukumiwa kwa kutegemea ushahidi usiothibitishwa wa mwathiriwa, kulikuwa na utata katika ushahidi wa mashahidi wa upande wa mashtaka, kesi ilitokana na mgogoro wa deni la Sh milioni mbili, hakukuwa na ushahidi wa DNA unaomhusisha na ujauzito, na kwamba alinyimwa mkalimani wa Kisukuma. Uamuzi wa Mahakama Baada ya kusikiliza hoja za pande zote, kupitia mwenendo wa kesi, Jaji Kafanabo amesema Mahakama ya kwanza ya rufaa ina wajibu wa kupitia upya ushahidi wote na kufikia hitimisho lake, huku akisisitiza kuwa katika kesi za jinai upande wa mashtaka unatakiwa kuthibitisha shtaka bila kuacha shaka yoyote. Mahakama imesema ushahidi wa mwathiriwa ulikuwa wa kuaminika na uliungwa mkono na ushahidi wa daktari aliyemfanyia uchunguzi na kuwasilisha Fomu ya Polisi Namba Tatu (PF3). Jaji amesema ushahidi wa baba wa mwathiriwa pamoja na maelezo ya mwathiriwa mwenyewe ulithibitisha kuwa alikuwa na umri wa miaka 16 wakati matukio hayo yalipotokea, hivyo kukidhi moja ya vipengele muhimu vya kosa la ubakaji wa mtoto chini ya miaka 18. Mahakama imesema sheria inaruhusu ushahidi wa mwathiriwa wa kosa la kingono kutegemewa hata bila uthibitisho mwingine endapo mahakama itajiridhisha kuwa ushahidi huo ni wa kweli na unaaminika. Jaji Kafanabo ameeleza kuwa mwathiriwa alitoa maelezo ya kina kuhusu namna alivyoshawishiwa kuingia katika uhusiano huo, maeneo walikokuwa wakikutana na nyakati walizokuwa wakifanya ngono, huku Makoye akishindwa kupinga ushahidi huo kwa kumuhoji wakati wa usikilizwaji wa kesi. Kutokana na hali hiyo, Mahakama iliridhika kuwa upande wa mashtaka ulithibitisha kosa la ubakaji bila kuacha shaka yoyote na hivyo hukumu ya miaka 30 jela ikaachwa kama ilivyotolewa na Mahakama ya Wilaya. Hata hivyo, kuhusu shtaka la kumpa mimba mwanafunzi, Mahakama ilisema pamoja na kuthibitika kuwa mwathiriwa alikuwa mwanafunzi wa Kidato cha Kwanza katika Shule ya Sekondari Mugango na kwamba alikuwa na ujauzito wa mwezi mmoja, ushahidi huo haukutosha kuthibitisha kuwa Makoye ndiye aliyesababisha ujauzito huo. Jaji amesema kwa kuwa Makoye alipinga kuhusika na ujauzito huo, upande wa mashtaka ulipaswa kuwasilisha ushahidi wa kisayansi wa DNA au ushahidi mwingine madhubuti unaounganisha mtuhumiwa na ujauzito huo, jambo ambalo halikufanyika. "Kwa mazingira ya kesi hii, shtaka la kumpa mimba mwanafunzi halikuthibitishwa bila kuacha shaka yoyote," imesema sehemu ya hukumu. Kutokana na hitimisho hilo, Mahakama ilifuta hatia na adhabu ya kosa la kumpa mimba mwanafunzi, lakini ikaamuru Makoye aendelee kutumikia kifungo cha miaka 30 jela kwa kosa la ubakaji.

This article was sourced from an external publication.

Share this article

Comments (0)

Want to join the discussion?

Sign in to post comments and engage with the community.

Be the first to comment!

DR Congo

View All
AD

Somalia

View All

Senegal

View All

Traditional Affairs

View All
AD
OneClick Africa Logo

Africa's premier digital hub for impactful news, entertainment, and business insights.

© 2026 OneClick Africa. All rights reserved.