TRENDING
Wanafamilia wanne wafariki dunia baada ya kunywa dawa ya kienyeji, mmoja ashikiliwa
Back to Home

Wanafamilia wanne wafariki dunia baada ya kunywa dawa ya kienyeji, mmoja ashikiliwa

Mwananchi about 2 hours 2 mins read
Moshi. Jeshi la Polisi Mkoa wa Kilimanjaro linamshikilia Beatrice Urassa (59), kwa tuhuma za kuhusika na vifo vya watu wanne wa familia moja baada ya kuwapa dawa ya kienyeji inayodaiwa kusababisha vifo vyao. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa, amethibitisha leo Julai 9, 2026 kutokea kwa tukio hilo katika Kitongoji cha Kinyaro, Kata ya Mnadani, Wilaya ya Hai. Amesema uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa mtuhumiwa anadaiwa kuwapatia dawa ya kienyeji watu hao Julai 5, 2026, kabla ya hali zao kuzorota na baadaye kufariki dunia walipokuwa wakipatiwa matibabu katika Hospitali ya Machame na Hospitali ya Wilaya ya Hai. Kamanda Maigwa amewataja waliofariki dunia kuwa ni Hamida Kweka (26), Robson Meena (34), Ismail Uronu (34) na Kamama Uronu (45). "Ni kweli kwamba Julai 5, 2026, katika Kitongoji cha Kinyaro, Kata ya Mnadani, Wilaya ya Hai, watu wanne wa familia moja walifariki dunia baada ya kunywa dawa ya kienyeji." “Walifariki wakiwa wanapatiwa matibabu katika Hospitali ya Machame na Hospitali ya Wilaya ya Hai," amesema. Amesema uchunguzi wa awali umebaini kuwa mtuhumiwa anadaiwa kuwapatia dawa hiyo ya kienyeji watu hao, huku chanzo na mazingira ya tukio hilo yakiendelea kuchunguzwa. "Jeshi la Polisi Mkoa wa Kilimanjaro linaendelea na uchunguzi kuhusu tukio hili. Uchunguzi utakapokamilika, hatua nyingine za kisheria zitachukuliwa," amesema Kamanda Maigwa.

This article was sourced from an external publication.

Share this article

Comments (0)

Want to join the discussion?

Sign in to post comments and engage with the community.

Be the first to comment!

DR Congo

View All

Somalia

View All
AD

Senegal

View All

Traditional Affairs

View All
AD
OneClick Africa Logo

Africa's premier digital hub for impactful news, entertainment, and business insights.

© 2026 OneClick Africa. All rights reserved.