TRENDING
Barcelona cancel Morocco friendly over border crisis • Fayose inaugurated as chairman of Rural Electrification Agency • Threat against the President can't be described as exercise of free speech — Prof. Beyuo to NPP • Jailed Wontumi still in NPP national chairmanship race — Dr Palgrave Boakye-Danquah • 'Failure to stop galamsey will make August 6 deaths meaningless' — Solomon Owusu • Mahama reshuffles cabinet, nominates Zanetor Rawlings and Mahama Ayariga to Environment and Local Government Ministries • Cynthia Morgan backs Peter Okoye, says artistes often suffer in silence • COAS warns soldiers against substance abuse, stresses mental health • Nigeria’s learning crisis is bigger than its schooling crisis • How a Lagos startup turned failed OTPs into a $5.3m African infrastructure business • Paint makers boost margins on lower input costs in H1 • 24 Nigerian companies join NGX trillionnaire club • Kano rejects conversion of Jambulo afforestation complex to private plots • Friday Sermon: Beware, the flesh of Islamic scholars (Ulama’) is poisonous!, By Murtadha Gusau • DTN@100 Heroes Awards Honour National Devt, Sustainability, Social Impact, National Global Champion Award Recipients • Askofu Amani: Kiburi, ukaidi kwa vijana vinaliangamiza Taifa • Man City reject Barcelona bid for Rodri – Reports • 2027: Youths, students rally behind Tinubu, Abiodun, Adeola in Ogun • Court to rule on Zamfara APC primaries dispute August 31 • Court fixes August 31 for judgment in Shinkafi’s suit against APC, INEC • Barcelona cancel Morocco friendly over border crisis • Fayose inaugurated as chairman of Rural Electrification Agency • Threat against the President can't be described as exercise of free speech — Prof. Beyuo to NPP • Jailed Wontumi still in NPP national chairmanship race — Dr Palgrave Boakye-Danquah • 'Failure to stop galamsey will make August 6 deaths meaningless' — Solomon Owusu • Mahama reshuffles cabinet, nominates Zanetor Rawlings and Mahama Ayariga to Environment and Local Government Ministries • Cynthia Morgan backs Peter Okoye, says artistes often suffer in silence • COAS warns soldiers against substance abuse, stresses mental health • Nigeria’s learning crisis is bigger than its schooling crisis • How a Lagos startup turned failed OTPs into a $5.3m African infrastructure business • Paint makers boost margins on lower input costs in H1 • 24 Nigerian companies join NGX trillionnaire club • Kano rejects conversion of Jambulo afforestation complex to private plots • Friday Sermon: Beware, the flesh of Islamic scholars (Ulama’) is poisonous!, By Murtadha Gusau • DTN@100 Heroes Awards Honour National Devt, Sustainability, Social Impact, National Global Champion Award Recipients • Askofu Amani: Kiburi, ukaidi kwa vijana vinaliangamiza Taifa • Man City reject Barcelona bid for Rodri – Reports • 2027: Youths, students rally behind Tinubu, Abiodun, Adeola in Ogun • Court to rule on Zamfara APC primaries dispute August 31 • Court fixes August 31 for judgment in Shinkafi’s suit against APC, INEC
Wanywaji waeleza umuhimu wa bia, wataka elimu zaidi
Back to Home

Wanywaji waeleza umuhimu wa bia, wataka elimu zaidi

Mwananchi about 3 hours 3 mins read
Dar es Salaam. Je, unajua kuwa leo ni siku maalumu kwa wapenda bia duniani kote? Umejiandaaje kusherehekea? Ndiyo, Siku ya Kimataifa ya Bia (IBD) husherehekewa Ijumaa ya kwanza ya Agosti kila mwaka ambapo kwa mwaka huu imeangukia Agosti 7. Watu hukusanyika kwenye klabu za usiku, baa, vioski vya mangi au majumbani kunywa bia huku wakitoa shukrani kwa wahudumu wa baa, wauzaji na hata wazalishaji w akinywaji hicho pendwa. Iwe bia yako imechachushwa au la, ni nyeusi au nyepesi, ina ladha kali, chungu, laini, au ni ya ndani au nje ya nchi, ungana na wengine kuinua glasi zenu kuadhimisha siku hii. Maadhimisho ya siku hii yalianzia huko Santa Cruz, California nchini Marekani, mwaka 2007. Hadi sasa siku hii inasherehekewa katika miji 207, katika nchi 50 duniani zilizotawanyika katika mabara sita. Kila jamii duniani ina aina yake ya bia na historia inaonyesha kinywaji hiki kilianza kutengenezwa kisasa katika karne ya 18, hata hivyo, kabla ya hapo zilikuwepo pombe mbalimbali zilizokuwa zikitengenezwa kienyeji kutokana na teknolojia kuwa duni. Licha ya hatari ambazo zimekuwa zikijitokeza miaka ya karibuni, bia imekuwa ni kinywaji ambacho kinawaunganisha watu na kuimarisha umoja wao huku wakifurahia maisha yao bila kusumbua wengine. Wanywaji mbalimbali waliozungumza na Mwananchi wanaeleza kwamba kinywaji hicho kimekuwa kiungo muhimu katika ustawi wa maisha ya jamii, hivyo kinatakiwa kutazamwa kwa namna chanya badala ya kudhibitiwa. Hata hivyo, baadhi wanaeleza haja kwa Serikali kuongeza nguvu katika kudhibiti bia bandia zinazozalishwa au kuingizwa nchini kinyume cha sheria, kwani zinasababisha matatizo katika afya za watu. Mmoja wa wanywaji wa bia, mkazi wa Dar es Salaam, Joyce Kibiki ametoa ushauri kwa watengenezaji wa bia kuangalia uingizwaji wa bia feki ambazo siyo tu zinaathiri afya za wanywaji, bali pia zinaharibu soko la bidhaa zao. “Serikali ione kinywaji hiki kama nyenzo muhimu katika kujenga umoja na Amani, hivyo iache kuongeza kodi mara kwa mara, jambo linalofanya wazalishaji nao waongeze bei bia mitaani,” amesema Joyce. Kwa upande wake, Miriam Juakali amesema wanywaji wa bia ni watu wenye upendo kwa sababu wengi wanaokunywa pamoja baa wanakuwa hawajuani, lakini wanakaa na kuzungumza kwa upendo kama vile wamefahamiana miaka mingi. “Siku hii ipo kwa ajili ya kudumisha upendo, bia ndiyo kinywaji kinachowakutanisha watu na kujenga umoja na kudumisha amani. Kwa hiyo, siku hii ni muhimu kwani kinatukumbusha umoja unaojengwa kwenye mazungumzo tukiwa na bia mezani,” amesema. Mwanamke huyo anatoa wito kwa Serikali kuacha kuongeza kodi kwenye bia kwani unywaji wa kawaida hauna athari kama ilivyo kwa wanywaji wa pombe kali. Amesisitiza haja ya wanywaji wenyewe kunywa kistaarabu ili kulinda afya zao na kujiepusha na vitendo viovu. Mkazi wa Moshi mkoani Kilimanjaro, Derrick Njau amesema pamoja na faida zake katika jamii, wanywaji wa bia wamekuwa wakikabiliwa na vitisho hasa kuwepo kwa bia feki, na wengine hawataki kunywa bia zilizotengenezwa siku za karibuni. Pia, Njau amesema bia za nje ni za kuchukuliwa kwa umakini kwa sababu baadhi yake ni feki na zinaweza kusababisha madhara kwa kuwa nyingi hazijathibitishwa na Shirika la Viwango nchini (TBS). Mtumiaji huyo wa kinywaji hicho, amesema kunywa bia ni jambo moja, lakini kwenye unywaji huo kuna ‘connection’ nyingi zinapatikana kwa sababu kwenye baa ndiko watu wanazungumza mambo yao ya kimaisha na namna ya kujenga uchumi. “Elimu sahihi ya unywaji wa bia inatakiwa kutolewa kuhusu kiwango halisi cha bia ambacho mtu anatakiwa kunywa kwa siku. Siku hizi, bia ‘lite’ zinanyweka sana kwa sababu ni nyepesi na siyo chungu kama lager. Wataalamu watuambie, hizi nazo vipi,” amesema.

This article was sourced from an external publication.

Share this article
OneClick Africa Logo

Africa's premier digital hub for impactful news, entertainment, and business insights.

© 2026 OneClick Africa. All rights reserved.