TRENDING
Insecurity: Nigerian Defence Minister, Musa breaks silence on resignation rumour • Insecurity: How climate change is fueling conflict, displacing livelihoods across northern Nigeria • Measuring what matters: Why Nigeria scores 54.2 • The paying client, not just the needy • BusinessDay 21st Jul 2026 • Investing in fixed income • Nigeria must put its displaced citizens first • Get the write start • Akeredolu at 70: The man who trusted me with his voice, By Bámidélé Adémólá-Olátéjú • Yanayowasubiri wahitimu mitaani • 40 feared dead as boat carrying women, children capsizes in Jigawa • 2027: Kwankwaso confirms written one-term agreement with Obi • Reps begin clause-by-clause review of state police bill • Chanzo ghorofa kupigwa mnada kwa mkopo wa Sh10 milioni • Borrowing: Nigeria’s N80trn debt figure exaggerated – FG • How PFIPC got into  2026 Budget — Adeyemi • Solar lights up Nigeria’s Delta village, but rising demand is dimming it • WORLD IN BRIEF: Trump says Iran strikes honour fallen US troops, EU fines AliExpress €550m, Mali ambush kills over 50 and other stories • Petrol import habit returns despite Dangote’s growing output • Oil prices soar as attacks spread across Gulf energy routes • Insecurity: Nigerian Defence Minister, Musa breaks silence on resignation rumour • Insecurity: How climate change is fueling conflict, displacing livelihoods across northern Nigeria • Measuring what matters: Why Nigeria scores 54.2 • The paying client, not just the needy • BusinessDay 21st Jul 2026 • Investing in fixed income • Nigeria must put its displaced citizens first • Get the write start • Akeredolu at 70: The man who trusted me with his voice, By Bámidélé Adémólá-Olátéjú • Yanayowasubiri wahitimu mitaani • 40 feared dead as boat carrying women, children capsizes in Jigawa • 2027: Kwankwaso confirms written one-term agreement with Obi • Reps begin clause-by-clause review of state police bill • Chanzo ghorofa kupigwa mnada kwa mkopo wa Sh10 milioni • Borrowing: Nigeria’s N80trn debt figure exaggerated – FG • How PFIPC got into  2026 Budget — Adeyemi • Solar lights up Nigeria’s Delta village, but rising demand is dimming it • WORLD IN BRIEF: Trump says Iran strikes honour fallen US troops, EU fines AliExpress €550m, Mali ambush kills over 50 and other stories • Petrol import habit returns despite Dangote’s growing output • Oil prices soar as attacks spread across Gulf energy routes
CCWT yawaonya wafugaji Moshi kuingiza mifugo kwenye mashamba
Back to Home

CCWT yawaonya wafugaji Moshi kuingiza mifugo kwenye mashamba

Mwananchi about 14 hours 3 mins read
Moshi. Chama cha Wafugaji Tanzania (CCWT) Kanda ya Kaskazini, kimekemea vitendo vinavyodaiwa kufanywa na baadhi ya wafugaji vya kuingiza mifugo kwenye mashamba ya wakulima kwa nguvu na kuwashambulia wananchi wanaojaribu kuzuia uharibifu wa mazao, kikisisitiza kuwa vitendo hivyo ni makosa ya jinai na vinahatarisha amani. Kauli hiyo imekuja kufuatia malalamiko ya wakulima wa Kitongoji cha Sanya Line A, Kijiji cha Mabogini, Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro, wanaodai mifugo imekuwa ikiingia mashambani na kuharibu mazao yao, huku baadhi ya wananchi wakijeruhiwa katika makabiliano na wafugaji wanaodaiwa kutoka wilaya za Kiteto na Simanjiro kutafuta malisho. Kwa mujibu wa wakulima hao, changamoto hiyo imeendelea kwa takribani miaka mitano, ambapo mifugo huingia mashambani hasa kipindi cha mazao, na kusababisha hasara kubwa kwa wakulima. Mwenyekiti wa Kitongoji cha Sanya Line A, Thomas Ngonyani, amesema baadhi ya mifugo hiyo inaonekana kutoka nje ya Wilaya ya Moshi kutokana na chapa zilizopo kwenye miili ya ng'ombe kutofanana na zile zinazotumika katika eneo hilo. Akizungumza leo Jumatatu, Julai 20, 2026 kuhusu mgogoro huo, Naibu Katibu wa CCWT Kanda ya Kaskazini, Elifuraha Ndure amesema chama hicho hakitavumilia vitendo vinavyoweza kuvuruga uhusiano kati ya wakulima na wafugaji. “Kitendo cha kuingiza mifugo kwenye shamba la mtu kwa makusudi na kumshambulia anayelalamika ni kosa la jinai. Hatuwezi kuruhusu vitendo vinavyohatarisha usalama na amani ya wananchi,” amesema Ndure. Amesema ikiwa mfugaji anahitaji eneo la malisho, anapaswa kufuata taratibu zilizowekwa na kuzungumza na viongozi wa maeneo husika badala ya kutumia nguvu. Kuhusu madai ya baadhi ya wakulima kuwa wafugaji hujigamba kuwahonga viongozi na kushinda kesi kirahisi mahakamani, Ndure amevitaka vyombo vya dola kufanya uchunguzi wa kina na kuchukua hatua dhidi ya yeyote atakayebainika kuhusika na vitendo vya rushwa. Naye Mwenyekiti wa CCWT Kanda ya Kaskazini, inayojumuisha mikoa ya Kilimanjaro, Arusha na Manyara, Rumay Bajuta amesema kila Mtanzania ana haki ya kuhamia eneo lolote nchini, lakini anapaswa kuzingatia sheria na taratibu zilizowekwa. “Kuhama si kosa, lakini mfugaji anapofika eneo jipya anatakiwa kuripoti katika ofisi ya kijiji na kwa maofisa mifugo. Kulisha mifugo kwenye shamba la mtu au kumshambulia anayepinga ni uhalifu unaopaswa kuchukuliwa hatua za kisheria,” amesema. Awali, Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Godfrey Mnzava alisema Serikali inafahamu changamoto hiyo na kwamba baadhi ya mifugo hutoka maeneo ya nje ya wilaya, ikiwemo Simanjiro, na kuingia Moshi bila kufuata taratibu za uhamishaji. Amesema Serikali imekuwa ikitumia kamati za usuluhishi zinazowashirikisha wakulima na wafugaji kutafuta suluhu ya migogoro hiyo, huku akisisitiza kuwa matukio ya kushambuliwa kwa wananchi yanapaswa kushughulikiwa kama makosa ya jinai. CCWT Kanda ya Kaskazini imesema itakutana na viongozi wa wilaya pamoja na wafugaji waliopo katika maeneo yenye migogoro ili kutoa elimu kuhusu uzingatiaji wa sheria za vijiji na taratibu za uhamishaji wa mifugo, kwa lengo la kuzuia migogoro na kuimarisha mahusiano kati ya wafugaji na wakulima.

This article was sourced from an external publication.

Share this article

Comments (0)

Want to join the discussion?

Sign in to post comments and engage with the community.

Be the first to comment!

DR Congo

View All
AD

Senegal

View All

Somalia

View All
AD

Traditional Affairs

View All
OneClick Africa Logo

Africa's premier digital hub for impactful news, entertainment, and business insights.

© 2026 OneClick Africa. All rights reserved.